-
Kwa Nini Umwone Daktari wa Meno?Amkeni!—2007 | Mei
-
-
Jinsi Matatizo ya Meno Yanavyoanza
Madaktari wa meno wanaweza kukusaidia usipatwe na maumivu ya meno na using’olewe meno. Unaposhirikiana nao, madaktari hao wanaweza kuondoa madhara ya ukoga, ambao ni utando mwembamba wa bakteria unaonata kwenye meno. Bakteria hizo hula mabaki ya chakula. Zinabadili sukari kuwa asidi na kuvamia tabaka gumu la juu la meno (enamel), na kuifanya iwe na matundu. Matundu hayo yanapobomoka na kuwa shimo kubwa, jino huanza kuoza. Huenda usihisi chochote wakati huo, lakini jino linapooza kufikia sehemu zenye neva, unaweza kupata maumivu makali.
-
-
Kwa Nini Umwone Daktari wa Meno?Amkeni!—2007 | Mei
-
-
Kuzuia Kuharibika kwa Meno
Madaktari wa meno wanapendekeza uchunguzwe meno mara moja au mbili kwa mwaka, ikitegemea hali ya meno yako. Katika uchunguzi daktari atakupiga picha za eksirei, na kuchunguza meno yako kwa uangalifu ikiwa yameoza. Akitumia dawa za ganzi na mashine ya kutoboa, anaweza kuziba mashimo yoyote anayopata bila kukuumiza. Kwa wale ambao ni waoga sana, madaktari wachache sasa wanatumia mionzi ya leza au jeli ya kuyeyusha uozo, ambayo inaweza kupunguza au hata kufanya usihitaji kutobolewa. Kwa watoto, madaktari hao hukazia fikira sana meno yanayoanza kuota tena kuangalia kama yana nyufa kwenye sehemu ya juu ambayo itafanya iwe vigumu kusafisha kwa kutumia mswaki. Huenda madaktari wakapendekeza kufunika nyufa hizo kwa plastiki ya aina fulani ili kufanya iwe rahisi kuosha, na hivyo kuyalinda dhidi ya kuoza.
-