-
Uhuru wa Kusema Nyumbani—Je, Ni Hali Itishayo Kutokeza Matatizo?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
Uchunguzi uliofanywa na Shirika la Kisaikolojia la Marekani “hukadiria kwamba mtoto wa kawaida, mwenye kutazama televisheni kwa muda wa saa 27 kwa juma, ataona mauaji ya kimakusudi 8,000 na vitendo vya jeuri 100,000 tangu umri wa miaka 3 hadi 12,” likaripoti gazeti U.S.News & World Report. Je, wazazi wanaweza kihalali kudai kwamba hilo halina uvutano wowote kwa watoto wao? Au huenda likahusisha “hatari ya wazi na iliyopo”? Je, ni hapa ambapo kizuizi chapasa kuwekwa au mpaka kuwekwa kwa usemi huru?
Uchunguzi mmoja uliofanywa na wanasaikolojia wa chuo kikuu ulifunua kwamba wakati katuni za “mashujaa walio tayari kupigana sikuzote” zilipoonyeshwa kwa kikundi kimoja cha watoto wenye umri wa miaka minne na “katuni tulivu, zisizosisimua” kuonyeshwa kwa kikundi kingine, wale walioona mashujaa wa vituko walielekea sana kupiga na kutupa vitu baadaye. Wala athari za jeuri ya televisheni haififii baada ya utoto. Uchunguzi mwingine wa chuo kikuu, baada ya kufuatia watoto 650 tangu 1960 hadi 1995 na kuchunguza mazoea yayo ya utazamaji televisheni na mwenendo, ulipata kwamba wale waliotazama televisheni zenye jeuri mno wakiwa vijana walikua na kujihusisha katika mwenendo wenye ukali zaidi wakiwa watu wazima, kutia ndani kutendea vibaya wenzi wao wa ndoa na kuendesha gari wakiwa wamelewa.
-
-
Uhuru wa Kusema Nyumbani—Je, Ni Hali Itishayo Kutokeza Matatizo?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
Huenda wengine wakasababu kwamba jeuri ya televisheni na sinema huenda isichukuliwe kihalisi na watoto na kwamba sinema zote hizo zenye kuogofya hazina athari yoyote kwao. “Ikiwa ni hivyo,” likasema gazeti moja la habari la Uingereza, “kwa nini shirika moja la shule katika magharibi-kati ya Marekani lililazimika kuyaambia maelfu ya watoto kwamba hakukuwa na Kasa-Vigeuko Matineja wa Kininja katika mabomba ya maji machafu ya mahali hapo? Mashabiki hao wachanga wa Kasa walikuwa wakitambaa kuingia ndani ya mabomba hayo ili kuwatafuta, hiyo ndiyo sababu.”
-
-
Uhuru wa Kusema Nyumbani—Je, Ni Hali Itishayo Kutokeza Matatizo?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
Nyumbani kwapasa kuwa mahali salama kwa watoto, si mahali ambapo wanaweza kuwa windo rahisi kwa wale ambao wangewatumia kwa faida yao au vibaya, au mahali ambapo nyutu tulivu zaweza kuchochewa kudhihirisha hali za moyoni zenye jeuri. “Huenda ukahisi uhakikisho kwamba mtoto wako hatakuwa mwenye jeuri kamwe licha ya jeuri ya wakati wote ya televisheni,” akasema profesa wa chuo kimoja kikuu cha Marekani akiwahutubia wazazi. “Lakini huwezi kuwa na uhakikisho kwamba mtoto wako hatauawa kimakusudi au kulemazwa na mtoto wa mtu mwingine, aliyelelewa akitazama jeuri.” Kisha akasihi: “Kuwekewa mipaka utazamaji wa jeuri ya televisheni wa watoto kwapasa kuwa sehemu ya ajenda ya afya ya umma, pamoja na viti vya usalama, kofia za baiskeli, chanjo, na lishe bora.”
Ikiwa hungeruhusu mtu usiyemjua aje nyumbani kwako na kutumia lugha yenye matukano na kuzungumza kwa maneno machafu na mtoto wako kuhusu ngono na jeuri, basi usiruhusu redio na televisheni ziwe mtu huyo usiyemjua. Jua wakati wa kuizima au kubadili stesheni. Jua kile atazamacho mtoto wako, kwenye televisheni na kwenye kompyuta, hata katika usiri wa chumba chake. Ikiwa ajua kutumia kompyuta na kufikia mifumo ipatikanayo kwake, huenda ukashtuka kujua kile yeye huingiza akilini kila jioni. Ikiwa hukubali kile anachotazama mtoto wako, sema tu la na ueleze kwa nini. Hatakufa akizuiwa.
-