-
‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu la Mungu!Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
6. Kupimwa kwa hekalu kulimaanisha nini?
6 Sehemu hii ya ono ilimaanisha nini? Iliwahakikishia wahamishwa hao kwamba ibada safi ingerudishwa kabisa kwenye hekalu la Mungu. Na zaidi, kupimwa kwa hekalu kuliwapa uhakikisho kamili wa kimungu kwamba ono hilo lazima lingetimizwa. (Linganisha Yeremia 31:39, 40; Zekaria 2:2-8.) Ibada ya sanamu yote ingesafishwa iondolewe mbali. Yehova angeibariki nyumba yake mara nyingine tena.
Ukuhani na Yule Mkuu
7. Ni habari gani inayotolewa kuhusu Walawi na makuhani?
7 Ukuhani pia ungepitia hatua ya kusafishwa, au kutakaswa. Walawi wangepasa kukemewa kwa kukubali ibada ya sanamu, ilhali wana wa kikuhani wa Sadoki wangepongezwa na kuthawabishwa kwa kubaki safi.a Na bado, hivyo vikundi vyote viwili vingepata vyeo vya utumishi katika nyumba ya Mungu iliyorudishwa—ikitegemea, bila shaka, uaminifu wa mtu mmoja-mmoja. Zaidi, Yehova aliamuru: “Nao watawafundisha watu wangu tofauti iliyopo kati ya vitu vitakatifu na vitu vya sikuzote [“vichafu,” NW], na kuwafundisha kupambanua kati ya yaliyo machafu na yaliyo safi.” (Ezekieli 44:10-16, 23) Hivyo ukuhani ungerudishwa, na uvumilivu wenye uaminifu wa makuhani ungethawabishwa.
8. (a) Ni nani waliokuwa wakuu wa Israeli la kale? (b) Mkuu aliye katika ono la Ezekieli alikuwa mtendaji katika ibada safi kwa njia zipi?
8 Ono hilo pia humrejezea mmoja aitwaye mkuu. Tangu siku za Musa, taifa hilo lilikuwa na wakuu. Neno la Kiebrania linalotafsiriwa mkuu, yaani na·siʼʹ, lingeweza kurejezea kichwa cha jamaa ya upande wa baba, cha kabila, au hata cha taifa. Katika ono la Ezekieli, watawala wa Israeli wakiwa jamii wanakemewa kwa kuwaonea watu na wanahimizwa sana wasipendelee na wawe wenye haki. Ijapokuwa yeye si wa jamii ya kikuhani, mkuu huyo ni mtendaji kwa njia yenye kutokeza katika ibada safi. Yeye aingia na kutokea ua wa nje akiwa pamoja na yale makabila yasiyo ya kikuhani, aketi kwenye ukumbi wa Lango la Mashariki, na kuandaa baadhi ya dhabihu ili watu wazitoe. (Ezekieli 44:2, 3; 45:8-12, 17) Hivyo, ono hilo liliwahakikishia watu wa Ezekieli kwamba taifa lililorudishwa lingebarikiwa kwa kupewa viongozi wenye kielelezo kizuri, wanaume ambao wangetegemeza ukuhani katika kusimamia watu wa Mungu na kuwa vielelezo bora katika mambo ya kiroho.
Hiyo Nchi
9. (a) Nchi hiyo ingegawanywa vipi, lakini ni nani ambao hawangepata urithi? (b) Toleo takatifu lilikuwa nini, na ni nini ambacho kilikuwa humo?
9 Hatimaye, ono la Ezekieli lilitia ndani ukaguzi wa jumla wa nchi ya Israeli. Ingegawanywa, kila kabila lipate sehemu. Yule mkuu vilevile angepata urithi. Lakini makuhani hawangepata urithi, kwa kuwa Yehova alisema, “Mimi ni urithi wao.” (Ezekieli 44:10, 28; Hesabu 18:20) Ono hilo lilionyesha kwamba sehemu ya nchi iliyogawiwa yule mkuu ingekuwa kila upande wa eneo la pekee liitwalo toleo takatifu. Hilo lilikuwa kipande cha shamba chenye umbo la mraba kilichogawanywa katika sehemu tatu—ya juu kwa Walawi waliotubu, ya katikati kwa makuhani, na ya chini kwa ajili ya jiji na mashamba yake yenye kuzaa. Hekalu la Yehova lingekuwa katika sehemu ya shamba la makuhani, katikati mwa toleo lenye umbo la mraba.—Ezekieli 45:1-7.
10. Unabii uliohusu kugawanywa kwa nchi ulimaanisha nini kwa Wayahudi waaminifu waliokuwa uhamishoni?
10 Hayo yote ni lazima yawe yaliwatia moyo wahamishwa hao kama nini! Kila familia ilihakikishiwa kupata urithi nchini humo. (Linganisha Mika 4:4.) Ibada safi ingekuwa jambo kuu, lililokwezwa mahali hapo. Na ona kwamba katika ono la Ezekieli mkuu huyo, sawa na makuhani, angeishi katika sehemu ya nchi iliyotolewa na watu. (Ezekieli 45:16) Kwa hiyo, katika nchi iliyorudishwa, watu walipaswa kuchangia kazi ya wale ambao Yehova alichagua waongoze, wakiwaunga mkono kwa kukubali mwelekezo wao. Kwa ujumla, nchi hiyo ilikuwa mfano mzuri wa utaratibu, ushirikiano, na usalama.
11, 12. (a) Yehova anawahakikishiaje kiunabii watu wake kwamba angebariki nchi yao iliyorudishwa? (b) Miti iliyo kando-kando ya kingo za mto ilifananisha nini?
11 Je, Yehova angebariki nchi yao? Unabii huo wajibu swali hili kwa ufafanuzi wenye kuchangamsha moyo. Kijito kinatiririka kutoka hekaluni, nacho kinazidi kupanuka kiendeleapo, na kinakuwa mto kufikia wakati kiingiapo Bahari ya Chumvi. Humo baharini kinayapa uhai maji yasiyo na uhai, na biashara ya kuvua samaki yasitawi kando-kando ya eneo la ufuo. Kando-kando ya kingo za mto pana miti mingi inayozaa matunda mwaka mzima, yakitoa lishe na ponyo.—Ezekieli 47:1-12.
12 Kwa wahamishwa hao, ahadi hii ilirudia na kuthibitisha unabii wa mapema wa urudisho waliouthamini sana. Zaidi ya mara moja, manabii wa Yehova waliopuliziwa walikuwa wamelifafanua kwa maneno ya kiparadiso Israeli lililorudishwa na kukaliwa na watu tena. Kichwa kilichorudiwa-rudiwa kilihusu maeneo yenye ukiwa yakirudi kwenye uhai. (Isaya 35:1, 6, 7; 51:3; Ezekieli 36:35; 37:1-14) Hivyo basi, watu wangetarajia kwamba baraka za Yehova zenye kutokeza uhai zingetiririka kama mto kutoka kwenye hekalu lililorudishwa. Matokeo ni kwamba taifa lililokuwa limekufa kiroho lingekuwa hai. Watu hao waliorudishwa wangebarikiwa kwa kupewa wanaume wa kiroho wenye kutokeza—wanaume waadilifu na walio thabiti kama miti iliyo kando-kando ya kingo za kimaono za mto huo, wanaume ambao wangeongoza katika kujenga upya nchi iliyoharibiwa. Isaya pia alikuwa ameandika kuhusu “miti mikubwa ya haki” ambao ‘wangejenga upya mahali palipokuwa pameharibiwa kwa muda mrefu.’—Isaya 61:3, 4, NW.
-
-
‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu la Mungu!Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
12 Kwa wahamishwa hao, ahadi hii ilirudia na kuthibitisha unabii wa mapema wa urudisho waliouthamini sana. Zaidi ya mara moja, manabii wa Yehova waliopuliziwa walikuwa wamelifafanua kwa maneno ya kiparadiso Israeli lililorudishwa na kukaliwa na watu tena. Kichwa kilichorudiwa-rudiwa kilihusu maeneo yenye ukiwa yakirudi kwenye uhai. (Isaya 35:1, 6, 7; 51:3; Ezekieli 36:35; 37:1-14) Hivyo basi, watu wangetarajia kwamba baraka za Yehova zenye kutokeza uhai zingetiririka kama mto kutoka kwenye hekalu lililorudishwa. Matokeo ni kwamba taifa lililokuwa limekufa kiroho lingekuwa hai. Watu hao waliorudishwa wangebarikiwa kwa kupewa wanaume wa kiroho wenye kutokeza—wanaume waadilifu na walio thabiti kama miti iliyo kando-kando ya kingo za kimaono za mto huo, wanaume ambao wangeongoza katika kujenga upya nchi iliyoharibiwa. Isaya pia alikuwa ameandika kuhusu “miti mikubwa ya haki” ambao ‘wangejenga upya mahali palipokuwa pameharibiwa kwa muda mrefu.’—Isaya 61:3, 4, NW.
-