-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—IIMnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
47:1-5—Ni nini kinachofananishwa na maji ya mto ambao Ezekieli anaona katika maono? Maji hayo yanafananisha uandalizi wa Yehova kwa ajili ya uzima, kutia ndani dhabihu ya fidia ya Kristo Yesu na ujuzi juu ya Mungu unaopatikana katika Biblia. (Yeremia 2:13; Yohana 4:7-26; Waefeso 5:25-27) Kina cha mto huo kinazidi kuongezeka ili wapya wanaokubali ibada ya kweli wapate nafasi humo. (Isaya 60:22) Maji ya uzima ya mto huo yatatiririka kwa nguvu zaidi wakati wa ile Miaka Elfu, nayo yatatia ndani uelewaji zaidi unaotegemea vile “vitabu vya kukunja” vitakavyofunguliwa wakati huo.—Ufunuo 20:12; 22:1, 2.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezekieli—IIMnara wa Mlinzi—2007 | Agosti 1
-
-
47:9, 11. Ujuzi, ambao ni sehemu muhimu ya maji ya mfano, umekuwa ukiponya kwa njia ya ajabu katika siku zetu. Ujuzi huo unawapa uhai wa kiroho watu wanaoupata. (Yohana 17:3) Kwa upande mwingine, wale wasiokubali maji yanayoleta uzima ‘wataachwa kwenye chumvi,’ yaani, wataharibiwa milele. Ni muhimu kama nini ‘tufanye kabisa yote tunayoweza ili tulitumie sawasawa neno la kweli’!—2 Timotheo 2:15.
-