-
‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu la Mungu!Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
11, 12. (a) Yehova anawahakikishiaje kiunabii watu wake kwamba angebariki nchi yao iliyorudishwa? (b) Miti iliyo kando-kando ya kingo za mto ilifananisha nini?
11 Je, Yehova angebariki nchi yao? Unabii huo wajibu swali hili kwa ufafanuzi wenye kuchangamsha moyo. Kijito kinatiririka kutoka hekaluni, nacho kinazidi kupanuka kiendeleapo, na kinakuwa mto kufikia wakati kiingiapo Bahari ya Chumvi. Humo baharini kinayapa uhai maji yasiyo na uhai, na biashara ya kuvua samaki yasitawi kando-kando ya eneo la ufuo. Kando-kando ya kingo za mto pana miti mingi inayozaa matunda mwaka mzima, yakitoa lishe na ponyo.—Ezekieli 47:1-12.
12 Kwa wahamishwa hao, ahadi hii ilirudia na kuthibitisha unabii wa mapema wa urudisho waliouthamini sana. Zaidi ya mara moja, manabii wa Yehova waliopuliziwa walikuwa wamelifafanua kwa maneno ya kiparadiso Israeli lililorudishwa na kukaliwa na watu tena. Kichwa kilichorudiwa-rudiwa kilihusu maeneo yenye ukiwa yakirudi kwenye uhai. (Isaya 35:1, 6, 7; 51:3; Ezekieli 36:35; 37:1-14) Hivyo basi, watu wangetarajia kwamba baraka za Yehova zenye kutokeza uhai zingetiririka kama mto kutoka kwenye hekalu lililorudishwa. Matokeo ni kwamba taifa lililokuwa limekufa kiroho lingekuwa hai. Watu hao waliorudishwa wangebarikiwa kwa kupewa wanaume wa kiroho wenye kutokeza—wanaume waadilifu na walio thabiti kama miti iliyo kando-kando ya kingo za kimaono za mto huo, wanaume ambao wangeongoza katika kujenga upya nchi iliyoharibiwa. Isaya pia alikuwa ameandika kuhusu “miti mikubwa ya haki” ambao ‘wangejenga upya mahali palipokuwa pameharibiwa kwa muda mrefu.’—Isaya 61:3, 4, NW.
-
-
‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu la Mungu!Mnara wa Mlinzi—1999 | Machi 1
-
-
Wakuu, kama vile Nehemia na Zerubabeli, walitawala nchi hiyo bila upendeleo na kwa haki. Hekalu la Yehova lilirudishwa, na maandalizi yake kwa ajili ya uhai—yaani baraka za kuishi kupatana na agano lake—yakaanza kutiririka tena. (Kumbukumbu la Torati 30:19; Isaya 48:17-20) Moja ya baraka hizo ilikuwa ujuzi. Ukuhani ulirudishwa kwenye wajibu wake, na makuhani wakawafundisha watu Sheria. (Malaki 2:7) Tokeo ni kwamba watu walifanywa hai kiroho, wakawa tena watumishi wa Yehova wenye kuzaa matunda, kama ilivyofananishwa na kuponywa kwa Bahari ya Chumvi na kutokeza biashara ya uvuvi yenye matokeo.
-