-
Jinsi ya Kumkaribia “Msikiaji wa Sala”Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
9. Ni takwa gani lililopaswa kutimizwa ili kumkaribia Yehova kwa njia inayofaa katika patakatifu?
9 Katika Sheria ambayo Waisraeli walipewa, Yehova alitaja takwa la kumkaribia kwa njia inayokubalika katika patakatifu. Takwa gani? Kila asubuhi na kila jioni, zaidi ya kutoa matoleo ya wanyama, kuhani mkuu alipaswa kufukiza uvumba wenye manukato mbele za Yehova. Baadaye, hata makuhani wa cheo cha chini walifanya utumishi huo, isipokuwa katika Siku ya Upatanisho. Ikiwa makuhani hawangefanya tendo hilo la heshima, Yehova hangefurahia utumishi wao.—Kutoka 30:7, 8; 2 Mambo ya Nyakati 13:11.
-
-
Jinsi ya Kumkaribia “Msikiaji wa Sala”Mnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
Simulizi la Luka linatuambia kwamba wakati Zekaria, baba ya Yohana Mbatizaji, alipokuwa akifukiza uvumba katika patakatifu, umati wa waabudu wa Yehova ambao hawakuwa makuhani ulikuwa “ukisali nje.” Inaonekana kwamba ilikuwa desturi ya watu kukusanyika nje ya patakatifu ili kusali huku uvumba ukifukizwa mbele za Yehova kwenye madhabahu ya dhahabu.—Luka 1:8-10.
-