-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
Tunaweza Kudumisha Utimilifu!
16. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba wanadamu wanaweza kudumisha utimilifu kwa Mungu?
16 Tunaweza kuunga mkono enzi kuu ya Yehova na kudumisha utimilifu wetu, kwa sababu mtume Paulo aliandika hivi: “Hakuna jaribu ambalo limewapata ninyi ila lile lililo kawaida kwa watu. Lakini Mungu ni mwaminifu, naye hatawaacha ninyi mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili, bali pamoja na hilo jaribu ataifanya pia njia ya kutokea kusudi mweze kulivumilia.” (1 Kor. 10:13) Ni nini chanzo cha jaribu linalotajwa na Paulo, na Mungu anatufanyia jinsi gani njia ya kutokea?
-
-
Yehova Ni Bwana Wetu Mwenye Enzi Kuu!Mnara wa Mlinzi—2010 | Novemba 15
-
-
20, 21. Tunapojaribiwa, Mungu anafanya “njia ya kutokea” jinsi gani?
20 Yehova anafanya “njia ya kutokea” kwa kututia nguvu ili tushinde jaribu. Kwa mfano, watesaji wanaweza kututesa kimwili ili kujaribu kufanya tuikane imani yetu. Mateso kama hayo yanaweza kufanya tulegeze msimamo wetu ili kuepuka kupigwa zaidi, kuteswa, au labda kuuawa. Hata hivyo, kulingana na maneno ya Paulo yaliyoongozwa na roho ya Mungu na ambayo yanatupa uhakikisho katika 1 Wakorintho 10:13, tunajua kwamba hali inayosababisha jaribu ni ya muda tu. Yehova hataruhusu hali hiyo iendelee hivi kwamba tushindwe kubaki waaminifu kwake. Mungu anaweza kuitia nguvu imani yetu na kutupatia nguvu za kiroho tunazohitaji ili kudumisha utimilifu wetu.
21 Yehova anatutegemeza kupitia roho yake takatifu. Roho hiyo inatukumbusha pia mawazo ya Kimaandiko ambayo tunahitaji ili kushinda jaribu. (Yoh. 14:26) Kwa hiyo, hatudanganywi kufuata mwenendo mbaya. Kwa mfano, tunaelewa masuala yanayohusiana ya enzi kuu ya Yehova na utimilifu wa wanadamu. Wakiwa na ujuzi huo, watu wengi wamesaidiwa na Mungu kubaki waaminifu mpaka kifo. Lakini si kifo kilichowafanyia njia ya kutokea; Yehova ndiye aliyewasaidia kuvumilia mpaka mwisho bila kushindwa na jaribu. Yehova anaweza kutusaidia vivyo hivyo. Kwa kweli, anatumia pia malaika wake waaminifu ili kutusaidia wakiwa watumishi wa watu wote ‘wanaotumwa kuhudumu kwa ajili ya wale watakaorithi wokovu.’ (Ebr. 1:14)
-