Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Fulizeni Kuzaa Matunda Mengi’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 21]

      JINSI YA “KUZAA MATUNDA KWA UVUMILIVU”

      NI NINI hukusaidia kuendelea kuhubiri ujumbe wa Ufalme kwa uaminifu katika maeneo yasiyo na matokeo sana? Hapa pana majibu mazuri kwa swali hilo.

      “Kujua kwamba Yesu anatutegemeza kabisa hunitia moyo niwe na mtazamo mzuri na kuvumilia, hata hali iweje katika eneo.”—Harry, mwenye umri wa miaka 72; aliyebatizwa mwaka wa 1946.

      “Mimi hutiwa moyo na andiko la 2 Wakorintho 2:17. Andiko hilo linasema kwamba tunashiriki huduma ‘mbele ya Mungu, kwa ushirika na Kristo.’ Ninapokuwa shambani, ninafurahia kushirikiana na marafiki wangu bora zaidi.”—Claudio, mwenye umri wa miaka 43: aliyebatizwa mwaka wa 1974.

      “Kusema kweli, mimi huona ugumu sana kuhubiri. Hata hivyo, nimeona kwamba maneno haya yanayopatikana katika andiko la Zaburi 18:29 ni ya kweli: ‘Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.’”—Gerard, mwenye umri wa miaka 79; aliyebatizwa mwaka wa 1955.

      “Nikisoma andiko moja tu shambani, ninaridhika kuona kwamba mtu fulani alikubali moyo wake uchunguzwe na Biblia.”—Eleanor, mwenye umri wa miaka 26; aliyebatizwa mwaka wa 1989.

      “Mimi hujaribu kutumia tangulizi mbalimbali. Kuna tangulizi nyingi sana hivi kwamba siwezi kutumia zote katika miaka inayobaki ya maisha yangu.”—Paul, mwenye umri wa miaka 79; aliyebatizwa mwaka wa 1940.

      “Mimi sikasiriki watu wanapokataa kusikiliza. Mimi hujaribu kuwa mwenye urafiki, kuzungumza na watu na kusikiliza maoni yao.”—Daniel, mwenye umri wa miaka 75; aliyebatizwa mwaka wa 1946.

      “Nimekutana na watu waliobatizwa hivi karibuni ambao waliniambia kwamba kazi yangu ya kuhubiri iliwasaidia kwa kadiri fulani wawe Mashahidi. Sikujua kwamba mtu mwingine alijifunza Biblia pamoja nao na kuwasaidia wafanye maendeleo. Ninafurahi kujua kwamba tunafanya kazi ya kuhubiri kwa kushirikiana.”—Joan, mwenye umri wa miaka 66; aliyebatizwa mwaka wa 1954.

      Ni nini hukusaidia “kuzaa matunda kwa uvumilivu”?—Luka 8:15.

  • ‘Fulizeni Kuzaa Matunda Mengi’
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Februari 1
    • Kuzaa Matunda kwa Kueneza Mbegu ya Ufalme

      10. Kielezi cha Yesu cha mpanzi na aina mbalimbali za udongo kinaonyeshaje matunda ya Ufalme?

      10 Tunapata jibu katika kielezi cha Yesu cha mpanzi na aina mbalimbali za udongo. Jibu hilo linawatia moyo Mashahidi wanaohubiri maeneo yasiyo na matokeo sana. Yesu alisema kwamba mbegu ni ujumbe wa Ufalme unaopatikana katika Neno la Mungu, na kwamba udongo ni moyo wa mfano. Baadhi ya mbegu ‘zilianguka juu ya udongo mzuri, na, baada ya kuota, zikatokeza matunda.’ (Luka 8:8) Matunda gani? Baada ya bua la ngano kuota na kukomaa, linazaa matunda, yaani mbegu mpya, wala halizai mabua madogo ya ngano. Vivyo hivyo, matunda ambayo Mkristo hutokeza si lazima yawe ni wanafunzi wapya, bali ni mbegu mpya ya Ufalme.

      11. Matunda ya Ufalme yanaweza kufasiriwaje?

      11 Kwa hiyo, matunda si wanafunzi wapya wala sifa nzuri za Kikristo. Kwa kuwa mbegu inayopandwa ni neno la Ufalme, basi matunda ni mbegu zaidi za ufalme. Kwa habari hii, kuzaa matunda kunamaanisha kuzungumza juu ya Ufalme huo. (Mathayo 24:14) Je, sote tunaweza kuzaa matunda hayo ya Ufalme, yaani, kutangaza habari njema ya Ufalme hata hali zetu ziweje? Ndiyo! Katika kielezi hichohicho, Yesu anaeleza sababu.

      Kutoa Yaliyo Bora ili Kumtukuza Mungu

      12. Je, Wakristo wote wanaweza kuzaa matunda ya Ufalme? Eleza.

      12 ‘Kwa habari ya yule aliyepandwa juu ya udongo ulio bora, hutokeza, huyu mara mia, yule sitini, yule mwingine thelathini.’ (Mathayo 13:23) Huenda nafaka zilizopandwa shambani zisitokeze kiasi kilekile cha mazao ikitegemea hali. Vivyo hivyo, kwa sababu ya hali huenda yale tunayoweza kutimiza katika kutangaza habari njema yasilingane na ya wengine, na Yesu alionyesha kwamba anatambua jambo hilo. Huenda wengine wakawa na fursa zaidi, wengine wakawa na afya bora na nguvu zaidi. Hivyo, huenda tukafanya mengi au machache kuliko wengine. Hata hivyo, Yehova anafurahi iwapo tunatoa yaliyo bora zaidi. (Wagalatia 6:4) Hata ikiwa uzee au ugonjwa unaodhoofisha unatuzuia tusishiriki sana kazi ya kuhubiri, Yehova, Baba yetu mwenye huruma hutuhesabu miongoni mwa wale ‘wanaofuliza kuzaa matunda mengi.’ Kwa nini? Kwa sababu tunampa ‘vyote tulivyo navyo’—utumishi wa nafsi yote.b—Marko 12:43, 44; Luka 10:27.

      13. (a) Ni sababu gani kuu zaidi inayofanya ‘tuendelee na kufuliza’ kuzaa matunda ya Ufalme? (b) Ni nini kitakachotusaidia tuendelee kuzaa matunda katika maeneo yasiyo na matokeo sana? (Ona sanduku katika ukurasa wa 21.)

      13 Hata tuwe tunazaa matunda ya Ufalme kadiri gani, tutachochewa ‘tuendelee na kufuliza kuzaa matunda’ tunapokumbuka sababu ya kufanya hivyo. (Yohana 15:16) Yesu alitaja sababu kuu zaidi: “Baba yangu hutukuzwa katika hili, kwamba mfulize kuzaa matunda mengi.” (Yohana 15:8) Naam, kazi yetu ya kuhubiri hulitukuza jina la Yehova mbele ya watu wote. (Zaburi 109:30) Honor, Shahidi mwaminifu mwenye umri wa miaka 70 na kitu anasema: “Ni pendeleo kumwakilisha Aliye Juu Zaidi Sana, hata katika maeneo yasiyo na matokeo sana.” Wakati Claudio, Shahidi mwenye bidii tangu 1974, alipoulizwa kwa nini anaendelea kuhubiri hata ingawa ni wachache wanaoitikia katika eneo lao, alinukuu Yohana 4:34, ambapo tunasoma maneno haya ya Yesu: “Chakula changu ni kwamba mimi nifanye mapenzi yake aliyenituma na kumaliza kazi yake.” Claudio aliongeza kusema: “Kama Yesu, ningependa kuanza na pia kumaliza kazi yangu ya kutangaza Ufalme.” (Yohana 17:4) Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote wanakubaliana naye.—Ona sanduku “Jinsi ya ‘Kuzaa Matunda kwa Uvumilivu,’” katika ukurasa wa 21.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki