Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Familia ya Yehova Hufurahia Muungano Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
    • Utaratibu wa Kitheokrasi Ni wa Maana

      12. Ni nini sifa za familia yenye furaha na muungano, na ni mpango gani ulioendeleza muungano katika makutaniko ya Kikristo ya karne ya kwanza?

      12 Familia iliyo na uongozi thabiti bali wenye upendo na ambayo ni yenye utaratibu inaelekea kuwa yenye muungano na furaha. (Waefeso 5:22, 33; 6:1) Yehova ni Mungu wa utaratibu wenye amani, na wale wote walio katika familia yake humwona kuwa “Aliye juu.” (Danieli 7:18, 22, 25, 27; 1 Wakorintho 14:33) Wao hutambua pia kwamba amemweka rasmi Mwanae, Yesu Kristo, kuwa mrithi wa vitu vyote naye amemkabidhi mamlaka yote mbinguni na duniani. (Mathayo 28:18; Waebrania 1:1, 2) Kristo akiwa ndiye Kichwa, kutaniko la Kikristo ni tengenezo lenye utaratibu na lenye muungano. (Waefeso 5:23) Ili kusimamia utendaji mbalimbali wa makutaniko ya karne ya kwanza, kulikuwa na baraza linaloongoza ambalo washiriki walo walikuwa mitume na “wazee” wengine waliokuwa wakomavu kiroho. Makutaniko moja-moja yalikuwa na waangalizi, au wazee, na watumishi wa huduma waliowekwa rasmi. (Matendo 15:6; Wafilipi 1:1) Kuwatii wale walioongoza kuliendeleza muungano.—Waebrania 13:17.

      13. Yehova huvutaje watu, na ni nini matokeo ya kufanya hivyo?

      13 Lakini je, utaratibu huo wote unadokeza kwamba muungano wa waabudu wa Yehova unaweza kusemwa kuwa tokeo la uongozi thabiti, wenye ubaridi? Bila shaka la! Hakuna ukosefu wowote wa upendo kwa habari ya Mungu au tengenezo lake. Yehova huvuta watu kwa kuonyesha upendo, na kwa hiari na shangwe mamia ya maelfu kila mwaka hupata kuwa sehemu ya tengenezo la Yehova kwa kubatizwa kwa ufananisho wa kujiweka wakfu kwao kwa Mungu kwa moyo wote. Mtazamo wao wa akilini ni kama ule wa Yoshua, aliyewahimiza Waisraeli wenzake hivi: “Chagueni hivi leo mtakayemtumikia; . . . lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia BWANA.”—Yoshua 24:15.

      14. Kwa nini twaweza kusema kwamba tengenezo la Yehova ni la kitheokrasi?

      14 Tukiwa sehemu ya familia ya Yehova, sisi ni wenye shangwe na pia tuna usalama. Ni hivyo kwa sababu tengenezo lake ni la kitheokrasi. Ufalme wa Mungu ni theokrasi (kutokana na Kigiriki the·osʹ, mungu, na kraʹtos, utawala). Ni utawala wa Mungu, wenye kuagizwa rasmi na kusimamishwa naye. “Taifa takatifu” la Yehova lenye kutiwa mafuta linanyenyekea utawala wake na basi hilo pia ni la kitheokrasi. (1 Petro 2:9) Yule Theokrati Mkuu, Yehova, akiwa Hakimu, Mtoa-Sheria, na Mfalme wetu, twapaswa kuhisi tukiwa salama. (Isaya 33:22) Hata hivyo, namna gani ikiwa bishano fulani lingetokea na kutisha shangwe yetu, usalama wetu, na muungano wetu?

  • Familia ya Yehova Hufurahia Muungano Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
    • Tumikia kwa Muungano wa Kitheokrasi

      19. Kwa nini muungano umesitawi katika familia ya waabudu wa Yehova?

      19 Muungano husitawi washiriki wa familia wanaposhirikiana. Ndivyo ilivyo katika familia ya waabudu wa Yehova. Kwa kuwa watu wa kitheokrasi, wazee na wengine katika kutaniko la karne ya kwanza walimtumikia Mungu kwa kushirikiana kikamili na baraza linaloongoza, wakakubali maamuzi yalo. Kwa msaada wa baraza linaloongoza, wazee ‘walilihubiri neno’ na washiriki wa makutaniko kwa ujumla ‘wakanena mamoja.’ (2 Timotheo 4:1, 2; 1 Wakorintho 1:10) Kwa hiyo kweli zilezile za Kimaandiko zilitolewa katika huduma na kwenye mikutano ya Kikristo, iwe ni katika Yerusalemu, Antiokia, Roma, Korintho, au kwingineko. Muungano wa kitheokrasi wa aina hiyo uko leo.

      20. Ili kuhifadhi muungano wetu wa Kikristo, ni lazima tufanye nini?

      20 Ili kuhifadhi muungano wetu, sisi sote tulio sehemu ya familia ya Yehova ya tufeni pote twapaswa kujitahidi kuonyesha upendo wa kitheokrasi. (1 Yohana 4:16) Twahitaji kunyenyekea mapenzi ya Mungu na kuonyesha staha yenye kina kuelekea ‘mtumwa mwaminifu’ na Baraza Linaloongoza. Bila shaka utii wetu ni wa hiari na wenye shangwe, sawa na wakfu wetu kwa Mungu. (1 Yohana 5:3) Mtunga-zaburi alifungamanisha shangwe na utii kwa njia ifaayo kama nini? Aliimba hivi: “Haleluya. Heri [“Mwenye furaha ni,” NW] mtu yule amchaye BWANA, apendezwaye sana na maagizo yake.”—Zaburi 112:1.

      21. Twaweza kujithibitishaje kuwa watu wa kitheokrasi?

      21 Yesu, Kichwa cha kutaniko, ni mtu wa kitheokrasi kikamili na sikuzote hufanya mapenzi ya Baba yake. (Yohana 5:30) Basi, acheni tufuate Kielelezo chetu kwa kufanya mapenzi ya Yehova kwa njia ya kitheokrasi na kwa muungano tukishirikiana kikamili na tengenezo Lake. Ndipo kwa shangwe na shukrani ya kuhisiwa moyoni, twaweza kurudia wimbo huu wa mtunga-zaburi: “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja, kwa umoja [“muungano,” NW].”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki