-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inafanywa baada ya Funzo la Biblia la Kutaniko. Mkutano huo wa dakika 30 umekusudiwa kuwasaidia Wakristo wasitawishe “ufundi wa kufundisha.” (2 Timotheo 4:2) Kwa mfano, je, mtoto wako au rafiki amewahi kukuuliza swali kumhusu Mungu au Biblia na ikawa vigumu kwako kumjibu vizuri? Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inaweza kukufundisha jinsi ya kujibu maswali magumu kwa njia yenye kutia-moyo, kutoka katika Biblia. Hivyo, tunaweza kusema kama nabii Isaya ambaye alisema hivi: “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amenipa ulimi wa waliofundishwa, ili nijue jinsi ya kumjibu neno yeye aliyechoka.”—Isaya 50:4.
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inaanza kwa hotuba inayotegemea sehemu ya Biblia ambayo wale waliohudhuria walitiwa moyo wasome juma lililotangulia. Baada ya hotuba hiyo, msemaji anawaomba wahudhuriaji watoe maelezo mafupi kuhusu mambo waliyofaidika nayo katika usomaji huo. Baada ya mazungumzo hayo, wanafunzi ambao wamejiandikisha katika shule hiyo wanatoa migawo waliyopewa.
Wanafunzi wanagawiwa kusoma sehemu fulani ya Biblia wakiwa jukwaani au waonyeshe jinsi ya kumfundisha mtu habari fulani ya Biblia. Baada ya kila hotuba, mshauri mwenye uzoefu anampongeza mwanafunzi kuhusu jambo alilofanya vizuri, akitoa maelezo yake kwenye kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Baadaye, wakiwa faraghani, anaweza kumpa mwanafunzi mapendekezo ya kuboresha ufundishaji wake.
Sehemu hiyo yenye kusisimua imekusudiwa kuwasaidia wanafunzi na pia wote waliohudhuria wanaotaka kuwa wasomaji, wasemaji, na wafundishaji bora. Baada ya Shule hiyo ya Huduma ya Kitheokrasi kumalizika, wimbo unaotegemea andiko la Biblia unaanzisha Mkutano wa Utumishi.
-
-
Unaalikwa kwa UchangamfuMnara wa Mlinzi—2009 | Februari 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 22]
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-