-
Miongozo ya Waangalizi wa ShuleFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Kutumia Fomu ya Mashauri. Fomu ya mashauri ya kila mwanafunzi iko katika kitabu chake mwenyewe cha shule kwenye ukurasa wa 79 hadi 81. Kama inavyoonyeshwa na rangi tofauti-tofauti, mwanafunzi anapokuwa na mgawo wa kusoma anaweza kupewa shauri lolote kuanzia shauri la 1 hadi 17. Wakati wa kutoa onyesho, wanafunzi wanaweza kutumia shauri lolote ila 7, 52, na 53. Mashauri yote yanaweza kutumiwa kwa hotuba ila 7, 18, na 30.
Mwanafunzi anapopewa mgawo wa kushughulikia shauri fulani, mwangalizi wa shule anapaswa kuandika kwa penseli (kalamu ya risasi) sehemu ambayo imeandikwa “Tarehe ya Kupokea Mgawo” katika nafasi iliyoko kando ya shauri hilo kwenye fomu ya shauri katika kitabu cha mwanafunzi. Baada ya mwanafunzi kushughulikia mgawo wake, mwulize kwa faragha kama alifanya yale mazoezi ambayo yako mwishoni mwa shauri hilo. Ikiwa ndivyo, tia alama sanduku lililo katika fomu hiyo. Kama unapendekeza aendelee kufanyia kazi shauri hilo, usiandike jambo lolote katika fomu yake ya shauri; usijaze ile nafasi ya “Tarehe Uliotimizwa.” Unapaswa kutia alama sehemu hiyo wakati tu mwanafunzi yu tayari kufanyia kazi shauri jingine. Kwa kuongezea, kwenye ukurasa wa 82 wa kitabu cha mwanafunzi, baada ya kila hotuba ya mwanafunzi, andika tarehe upande wa kushoto wa kikao ambacho mwanafunzi ametumia. Kuna nafasi katika fomu ya mashauri na kwenye orodha ya vikao ya kuruhusu kila kikao kitumiwe mara mbili. Wanafunzi wanapaswa kuja na vitabu vyao shuleni.
Toa mgawo wa shauri moja tu la usemi kwa wakati mmoja. Kwa kawaida ni vizuri kushughulikia mashauri kama yanavyofuatana kwenye orodha. Lakini wanafunzi wengine wakionyesha uwezo mkubwa, unaweza kuwatia moyo wajifunze na kutumia mashauri fulani peke yao. Kisha unaweza kuwasaidia kutimiza mashauri ambayo unaona yataboresha sana uwezo wao wakiwa wasemaji na walimu stadi.
Hata kama mwanafunzi amekuwa katika shule kwa miaka mingi, bado anaweza kufaidika sana akijifunza kila somo na kulitumia. Ili uwasaidie wanafunzi wenye mahitaji hususa, unaweza kuchagua sifa fulani za usemi ambazo wanaweza kufanyia kazi badala ya kufuata kila shauri kama lilivyoorodheshwa katika fomu ya shauri.
-
-
Miongozo ya Waangalizi wa ShuleFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Kumbuka kwamba wewe ni ‘mfanyakazi mwenzi’ wa akina ndugu na dada. (2 Kor. 1:24) Hata wewe pia unahitaji kuendelea kutia bidii kuwa msemaji na mwalimu stadi. Jifunze kitabu Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, tumia mashauri yake, na uweke mfano mzuri kwa wengine.
Fanya hivyo kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wawe wasomaji wazuri, wasemaji bora, na walimu stadi. Ili ufaulu, jitahidi kuwasaidia wanafunzi inapohitajika ili waelewe sifa mbalimbali za usemi, umuhimu wake, na jinsi ya kuzikuza. Kitabu hiki kimetayarishwa kwa njia ambayo itakusaidia kutimiza kusudi hilo. Unahitaji kufanya mengi zaidi mbali na kukisoma tu kitabu hiki. Fafanua mawazo ya kitabu hiki na kuonyesha jinsi ya kuyatumia.
-
-
Miongozo ya Waangalizi wa ShuleFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Watajie wanafunzi wasome shauri watakalofanyia kazi siku chache baada ya kupokea mgawo huo. Watie moyo watumie yale wanayojifunza wanapotayarisha migawo kwa ajili ya shule, katika mazungumzo ya kawaida, wanapotoa maelezo katika mikutano, na katika utumishi wa shambani.
-