-
Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa TimotheoMnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
KUTANIKO jipya huko Thesalonike lilipatwa na upinzani tangu lilipoanzishwa wakati mtume Paulo alipotembelea huko. Kwa hiyo, Timotheo—labda akiwa na umri wa miaka 20 na kitu—anaporudi kutoka Thesalonike akiwa na ripoti nzuri, Paulo anachochewa kuwaandikia Wathesalonike barua ili kuwapongeza na kuwatia moyo. Barua hiyo ambayo inaelekea iliandikwa mwishoni mwa mwaka wa 50 W.K., ndiyo ya kwanza kati ya maandishi ya Paulo yaliyoongozwa na roho ya Mungu.
-
-
Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa TimotheoMnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
“TUKAE MACHO”
Paulo anawapongeza Wathesalonike kwa ‘kazi yao ya uaminifu, kazi yao ya jasho yenye upendo, na uvumilivu wao.’ Anawaambia kwamba wao ni ‘tumaini, shangwe, na taji lake la furaha.’—1 The. 1:3; 2:19.
Baada ya kuwatia moyo Wakristo wa Thesalonike wafarijiane na tumaini la ufufuo, Paulo anasema hivi: “Siku ya Yehova inakuja sawasawa kabisa kama mwizi usiku.” Anawashauri ‘wakae macho’ na kutunza akili zao.—1 The. 4:16-18; 5:2, 6.
Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:
4:15-17—Ni nani ‘wanaonyakuliwa katika mawingu ili kukutana na Bwana hewani,’ na hilo linatukia jinsi gani? Hao ni Wakristo watiwa-mafuta ambao wanaishi wakati wa kuwapo kwa Kristo katika mamlaka ya Ufalme. ‘Wanakutana na Bwana’ Yesu katika makao yasiyoonekana ya kimbingu. Hata hivyo, ili wakutane na Bwana huko, wanapaswa kwanza kufa na kufufuliwa wakiwa viumbe wa roho. (Rom. 6:3-5; 1 Kor. 15:35, 44) Kuwapo kwa Kristo tayari kumeanza, hivyo Wakristo watiwa-mafuta wanaokufa leo hawabaki wakiwa wafu. ‘Wananyakuliwa,’ au kufufuliwa papo hapo.—1 Kor. 15:51, 52.
5:23—Paulo alimaanisha nini aliposali kwamba ‘roho na nafsi na mwili wa akina ndugu vihifadhiwe’? Paulo alikuwa akizungumza kuhusu roho, nafsi, na mwili ambao unafanyizwa na washiriki wote wa kutaniko la Kikristo, nao ulitia ndani Wakristo watiwa-mafuta huko Thesalonike. Badala ya kusali tu kwamba kutaniko lihifadhiwe, alisali kwa ajili ya kuhifadhiwa kwa “roho” ya kutaniko, au mwelekeo wa akili wa kutaniko. Pia, alisali kwa ajili ya “nafsi” ya kutaniko, yaani, uhai wa kutaniko, au kuwepo kwa kutaniko, na kwa ajili ya “mwili” wa kutaniko—mwili ambao unafanyizwa na Wakristo watiwa-mafuta. (1 Kor. 12:12, 13) Hivyo, sala hiyo inaonyesha jinsi Paulo alivyohangaikia sana kutaniko.
Mambo Tunayojifunza:
1:3, 7; 2:13; 4:1-12; 5:15. Njia yenye matokeo ya kutoa shauri ni kumpongeza mtu kwa unyoofu na pia kumtia moyo afanye vizuri zaidi.
4:1, 9, 10. Waabudu wa Yehova wanapaswa kuendelea kufanya maendeleo ya kiroho.
5:1-3, 8, 20, 21. Siku ya Yehova inapokaribia, tunapaswa ‘kutunza akili zetu na kuvaa bamba la kifuani la imani na upendo na lile tumaini la wokovu kama kofia ya chuma.’ Zaidi ya hayo, tunapaswa kulikazia uangalifu sana Neno la Mungu la kinabii, Biblia.
-