-
Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa TimotheoMnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
Muda mfupi baadaye, anawaandikia Wakristo huko Thesalonike barua ya pili. Wakati huu, anasahihisha maoni yenye makosa ya watu fulani na anawahimiza akina ndugu kusimama imara katika imani.
-
-
Mambo Makuu Katika Barua kwa Wathesalonike na kwa TimotheoMnara wa Mlinzi—2008 | Septemba 15
-
-
“SIMAMENI IMARA”
Wakipotosha maana ya mambo ambayo Paulo alisema katika barua yake ya kwanza, inaelekea watu fulani katika kutaniko hilo wanapinga kwamba “kuwapo kwa Bwana” kunakaribia. Ili kusahihisha maoni hayo, Paulo anazungumza kuhusu mambo ambayo yanapaswa ‘kuja kwanza.’—2 The. 2:1-3.
Paulo anawahimiza hivi: “Simameni imara na mwendelee kuyashika mapokeo mliyofundishwa.” Anawaamuru ‘wajiepushe na kila ndugu anayetembea bila utaratibu.’—2 The. 2:15; 3:6.
Maswali ya Kimaandiko Yajibiwa:
2:3, 8—Ni nani “yule mtu wa uasi-sheria,” naye ataangamizwa jinsi gani? “Mtu” huyo anafananisha jamii ya makasisi wa dini zinazodai kuwa za Kikristo. Yule aliye na mamlaka ya kutangaza hukumu za Mungu juu ya waovu na kuamuru waangamizwe ni “Neno,” yaani, Msemaji Mkuu wa Mungu, Yesu Kristo. (Yoh. 1:1) Hivyo, inaweza kusemwa kwamba Yesu atamwangamiza yule mtu wa uasi-sheria “kwa roho [nguvu ya utendaji] ya kinywa chake.”
2:13, 14—Wakristo watiwa-mafuta ‘walichaguliwa tangu mwanzo kwa ajili ya wokovu’ jinsi gani? Watiwa-mafuta wakiwa jamii walikusudiwa au kuagizwa kimbele wakati Yehova alipokusudia uzao wa mwanamke uponde kichwa cha Shetani. (Mwa. 3:15) Pia, Yehova alitaja matakwa ambayo wanapaswa kutimiza, kazi ambayo wangefanya, na majaribu ambayo wangepata. Hivyo, aliwaita kwa ajili ya ‘lengo hilo.’
Mambo Tunayojifunza:
1:6-9. Yehova anatekeleza hukumu zake kwa kuwaangamiza waovu na kuwalinda watumishi wake.
3:8-12. Kukaribia kwa siku ya Yehova hakupaswi kutumiwa kuwa kisingizio cha kutofanya kazi ili kutosheleza mahitaji yetu na kujitegemeza wenyewe tunapoendelea kushiriki katika huduma. Kutofanya kazi kunaweza kutufanya tuwe wavivu na hivyo kuwa ‘wenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.’—1 Pet. 4:15.
-