Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuponda Kichwa cha Nyoka
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • na yeye ataenda nje kuongoza vibaya yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu, kukusanya hayo pamoja kwenye vita. Hesabu ya hawa ni kama mchanga wa bahari.

  • Kuponda Kichwa cha Nyoka
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Ufunuo 20:7-

  • Kuponda Kichwa cha Nyoka
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 21. Kwa jitihada yake ya mwisho, Shetani anaendeleaje, na kwa nini haipasi kutushangaza kwamba wengine watafuata Shetani hata baada ya Utawala wa Miaka Elfu?

      21 Jitihada ya mwisho ya Shetani itakuwaje? Yeye anadanganya “yale mataifa katika kona nne za dunia, Gogu na Magogu,” na kuyaongoza kwenye “vita.” Ni nani angeweza kuchukua upande wa Shetani baada ya miaka elfu moja ya utawala wa kitheokrasi wenye shangwe, wenye kujenga? Basi, usisahau kwamba Shetani aliweza kuongoza vibaya Adamu na Hawa wakamilifu walipokuwa wakifurahia uhai katika Paradiso ya Edeni. Na yeye aliweza kupotosha malaika wa kimbingu ambao walikuwa wameona matokeo mabaya ya uasi wa awali kabisa. (2 Petro 2:4; Yuda 6) Kwa hiyo tusishangae kwa vile baadhi ya wanadamu wakamilifu watarubuniwa wafuate Shetani hata baada ya utawala wa Ufalme wa Mungu wa miaka elfu wenye kupendeza.

      22. (a) Ni nini kinachoonyeshwa na usemi “yale mataifa katika kona nne za dunia”? (b) Kwa nini waasi huitwa “Gogu na Magogu”?

      22 Biblia huwaita waasi hawa “mataifa katika kona nne za dunia.” Hii haimaanishi kwamba aina ya binadamu itakuwa imekwisha gawanyikana-gawanyikana tena na kuwa mataifa yaliyo pekee. Inaonyesha tu kwamba hawa watajitenga wenyewe kutoka kwa wale washikamanifu, na waadilifu wa Yehova na kudhihirisha roho ile ile mbaya ambayo mataifa yanaonyesha leo. Wao ‘watafikiria njama yenye kudhuru,’ kama alivyofanya Gogu wa Magogu katika unabii wa Ezekieli, wakiwa na mradi wa kuharibu serikali ya kitheokrasi iliyo duniani. (Ezekieli 38:3, 10-12, NW) Kwa sababu hiyo, wao huitwa “Gogu na Magogu.”

      23. Ni nini kinachoonyeshwa na uhakika wa kwamba hesabu ya waasi ni “kama mchanga wa bahari”?

      23 Hesabu ya wale wanaojiunga na Shetani katika uasi wake itakuwa “kama mchanga wa bahari.” Huo ni wingi gani? Hakuna hesabu iliyotangulia kuwekwa rasmi. (Linga Yoshua 11:4; Waamuzi 7:12.) Hesabu ya mwisho yenye jumla ya waasi itategemea jinsi kila mtu mmoja mmoja atakavyotenda kwa kuitikia hila za ujanja za Shetani. Ingawa hivyo, pasi na shaka, watakuwa hesabu kubwa, kwa kuwa watahisi ni wenye nguvu vya kutosha kushinda “kambi ya watakatifu na jiji lenye kupendwa.”

      24. (a) Ni nini lililo “jiji lenye kupendwa” nalo linaweza kuzingirwaje? (b) Ni nini kinachowakilishwa na “kambi ya watakatifu”?

      24 “Jiji lenye kupendwa” lazima liwe jiji ambalo Yesu Kristo aliyetukuzwa anasema juu yalo kwa wafuasi wake kwenye Ufunuo 3:12 na ambalo yeye anaita “jiji la Mungu wangu, Yerusalemu jipya ambalo hushuka kutoka katika mbingu kutoka kwa Mungu wangu.” Kwa kuwa hili ni tengenezo la kimbingu, kani hizo za kidunia zingewezaje ‘kulizingira’? Ni kwa vile wao huzingira “kambi ya watakatifu.” Kambi huwa nje ya jiji; kwa hiyo, “kambi ya watakatifu” lazima iwakilishe wale walio duniani nje ya mahali pa kimbingu pa Yerusalemu Jipya ambao kwa ushikamanifu hutegemeza mpango wa Yehova wa kiserikali. Wakati waasi hao walio chini ya Shetani wanaposhambulia wale waaminifu, Bwana Yesu huona hilo kuwa ni shambulio juu ya yeye. (Mathayo 25:40, 45) “Yale mataifa” yatajaribu kufutilia mbali yote ambayo Yerusalemu Jipya la kimbingu limetimiza katika kufanya dunia paradiso. Hivyo kwa kushambulia “kambi ya watakatifu,” wao wanashambulia pia “jiji lenye kupendwa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki