-
Ujumbe Mtamu na MchunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Ngurumo Saba
7. Ni kwa jinsi gani malaika kabambe hupiga kilio kikuu, na ni nini maana ya kilio chake?
7 Fikirio la Yohana juu ya malaika kabambe huyu linakatizwa na huyo malaika mwenyewe: “Na yeye [huyo malaika] akapiga kilio kwa sauti kubwa kama vile wakati simba anaponguruma. Na wakati yeye alipopiga kilio kikuu, ngurumo saba zikatamka sauti zazo zenyewe.” (Ufunuo 10:3, NW) Mpaazo kama huo wenye nguvu ungedaka uangalifu wa Yohana, ukithibitisha kwamba kwa kweli Yesu ndiye “Simba ambaye ni wa kabila la Yuda.” (Ufunuo 5:5, NW) Pia Yohana angejua kwamba Yehova, vilevile, nyakati nyingine husemwa kuwa ‘hunguruma.’ Kunguruma kwa Yehova hutoa habari kiunabii ya kukusanywa kwa Israeli wa kiroho na kuja kwa “siku ya Yehova” ya uharibifu. (Hosea 11:10; Yoeli 3:14, 16; Amosi 1:2; 3:7, 8, NW) Kwa wazi, basi, ule mlio kama wa simba wa huyu malaika kabambe huonya kimbele juu ya matukio makubwa yanayofanana na hilo kwa ajili ya bahari na dunia. Unaita ngurumo saba ziseme.
8. Ni nini zilizo ‘sauti za ngurumo saba’?
8 Wakati uliotangulia Yohana amesikia sauti zikitoka katika kiti cha ufalme chenyewe cha Yehova. (Ufunuo 4:5) Huko nyuma katika siku ya Daudi, nyakati nyingine ngurumo halisi ilikuwa ikisemwa kuwa ni “sauti ya Yehova.” (Zaburi 29:3, NW) Wakati Yehova alipotangaza kwa sauti yenye kusikika kusudi lake la kutukuza jina lake mwenyewe katika siku za huduma ya kidunia ya Yesu, kwa wengi ilisikika kama ngurumo. (Yohana 12:28, 29) Kwa sababu hiyo, inapatana na akili nzuri kukata maneno kwamba ‘zile sauti za ngurumo saba’ ni tamko la Yehova mwenyewe la makusudi yake. Uhakika wa kwamba kulikuwa na ngurumo saba hudokeza ukamili wa yale ambayo Yohana alisikia.
9. Sauti kutoka katika mbingu inaamuru nini?
9 Lakini sikiliza! Sauti nyingine yatoka ikivuma. Inaleta amri ambayo lazima ionekane ngeni kwa Yohana: “Sasa wakati ngurumo saba ziliposema, mimi nilikuwa karibu kutaka kuandika; lakini mimi nikasikia sauti moja kutoka katika mbingu ikisema: ‘Tia kifungo vitu ambavyo ngurumo saba zilisema, na usiandike hivyo.” (Ufunuo 10:4, NW) Lazima Yohana awe alikuwa na hamu nyingi ya kusikia na kuandika jumbe hizo zenye ngurumo, kama vile jamii ya Yohana leo imengojea kwa hamu nyingi Yehova afumbue makusudi yake ya kimungu yachapwe. Mafunuo kama hayo huja tu katika wakati wa Yehova uliowekwa.—Luka 12:42; ona pia Danieli 12:8, 9.
-
-
Ujumbe Mtamu na MchunguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Sauti za ngurumo saba, zilizo na maonyo ya dhoruba yenye kuogofya zinazidi kuwa wazi na zenye sauti kubwa zaidi inapokaribia ile siku kuu ya Yehova ya kisasi.—Sefania 1:14-18.
-