-
Wahudumu wa Habari NjemaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
wakati ambapo unabii huu wa Isaya unatimia: “Mdogo atakuwa elfu, na mnyonge atakuwa taifa lenye nguvu. Mimi mwenyewe, Yehova, nitaharakisha jambo hilo kwa wakati wake.” (Ufu. 7:9, 14; Isa. 60:22) Ni heshima kubwa sana kuwa wahudumu wa habari njema katika siku hizi za mwisho!—Mt. 24:14.
-
-
Njia za Kuhubiri Habari NjemaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 9
Njia za Kuhubiri Habari Njema
YESU KRISTO alihubiri habari njema kwa bidii, akiwawekea mfano mzuri wafuasi wake. Alichukua hatua ya kuwatafuta watu, akizungumza nao na kuwafundisha nyumbani kwao na hadharani. (Mt. 9:35; 13:36; Luka 8:1) Yesu alizungumza na watu binafsi, aliwafundisha wanafunzi wake faraghani, na hata alihutubia maelfu ya watu. (Marko 4:10-13; 6:35-44; Yoh. 3:2-21) Alitumia kila pindi aliyopata kuwatia watu moyo na kuwapa tumaini. (Luka 4:16-19) Hakuacha nafasi ya kuhubiri impite hata alipohitaji kupumzika au kula. (Marko 6:30-34; Yoh. 4:4-34) Tunaposoma masimulizi ya huduma ya Yesu yaliyoongozwa na roho, je, hatuchochewi kuiga mfano wake? Bila shaka tunachochewa kumwiga, kama mitume walivyochochewa.—Mt. 4:19, 20; Luka 5:27, 28; Yoh. 1:43-45.
2 Fikiria nafasi ambazo Wakristo wanazo za kushiriki katika kazi iliyoanzishwa na Yesu Kristo miaka 2,000 hivi iliyopita.
KUHUBIRI NYUMBA KWA NYUMBA
3 Tukiwa Mashahidi wa Yehova tunatambua umuhimu wa kuhubiri habari njema ya Ufalme kwa utaratibu, yaani, nyumba kwa nyumba. Tumetumia sana njia hiyo hivi kwamba ni alama inayotutambulisha. Faida za kutumia njia hii ili kuwafikia mamilioni ya watu katika muda
-