-
Vitu Ambavyo Lazima Vitukie KaribuniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
4. (a) Kwa kuwa Yohana aliandika Ufunuo zaidi ya miaka 1,900 iliyopita, yeye angewezaje kusema juu ya “vitu ambavyo lazima vitukie karibuni”? (b) Ithibati inaonyesha nini sasa juu ya vitu vilivyotabiriwa?
4 Ingawa hivyo, Yohana angewezaje kusema, hawa “watumwa” wangeonyeshwa “vitu ambavyo lazima vitukie karibuni”? Je! maneno hayo hayakusemwa zaidi ya miaka 1,900 iliyopita? Kwa maoni ya Yehova, ambaye machoni pake miaka elfu moja ni “kama siku ya jana,” miaka 1,900 ni wakati mfupi unapolinganishwa na vipindi virefu vya wakati aliotumia katika kuumba na kutayarisha dunia ikaliwe na wanadamu. (Zaburi 90:4) Mtume Paulo aliandika juu ya “taraja na tumaini lenye hamu nyingi” lake mwenyewe, kwa kuwa pasipo shaka uhakika wa thawabu yake ulionekana kwake kuwa karibu sana. (Wafilipi 1:20, NW) Hata hivyo, leo, ithibati ni tele kwamba vile vitu vyote vilivyotabiriwa vitatukia kwa wakati ulioorodheshwa. Wokovu wenyewe wa aina ya binadamu haujapata kamwe kuhatarishwa kabla ya sasa katika historia. Ni Mungu tu aliye na ufumbuzi!—Isaya 45:21.
-
-
Vitu Ambavyo Lazima Vitukie KaribuniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Ufunuo kwa Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa, aonyeshe watumwa wake vitu ambavyo lazima vitukie karibuni.” (Ufunuo 1:1a, NW)
-