Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wakati na Umilele Tunajua Nini Hasa Kuzihusu?
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • Biblia hutaja wakati kuwa halisi, hata ingawa haiufafanui. Kwanza, Biblia hutuambia kwamba Mungu aliumba “mianga”—jua, mwezi, na nyota— iwe alama za wakati, ili “iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka.” Matukio mengi yaliyoandikwa katika Biblia yanafuata kabisa mkondo wa wakati. (Mwanzo 1:14; 5:3-32; 7:11, 12; 11:10-32; Kutoka 12:40, 41) Biblia pia hutaja wakati kuwa kitu ambacho twapaswa kutumia kwa hekima ili tuweze kupata baraka za Mungu za wakati wa umilele—taraja la kuishi milele.—Waefeso 5:15, 16.

  • Mungu Si wa Polepole kwa Habari ya Ahadi Yake
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Juni 1
    • Katika karne ya kwanza, kuna watu fulani ambao yaonekana walihisi kwamba Mungu angelipasa kuwa ametimiza ahadi zake mapema zaidi. Walikosa subira sana hivi kwamba hata walimwona Mungu kuwa wa polepole au mwenye kuchelewa. Kwa sababu hiyo, mtume Petro alilazimika kuwakumbusha kwamba maoni ya Mungu kuhusu wakati ni tofauti sana na yetu. Petro aandika hivi: “Acheni jambo hili moja lisiwe likiponyoka kujali kwenu, kwamba siku moja kwa Yehova ni kama miaka elfu na miaka elfu kama siku moja.”—2 Petro 3:8.

      Kulingana na njia hiyo ya kukadiria wakati, mtu mwenye umri wa miaka 80 ameishi kwa muda upatao saa mbili tu, nayo historia yote ya wanadamu imechukua muda upatao siku sita tu. Tukitazama mambo kwa njia hiyo, inakuwa rahisi zaidi kwetu kuelewa njia ya Mungu ya kushughulika nasi.

      Hata hivyo, Mungu si asiyejali wakati. Kinyume cha hilo, yeye yuko chonjo sana kuhusu wakati. (Matendo 1:7) Kwa hiyo, Petro anaendelea kusema hivi: “Yehova si wa polepole kwa habari ya ahadi yake, kama watu fulani waonavyo kuwa ni upolepole, bali yeye ni mwenye subira kwenu kwa sababu hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Petro 3:9) Tofauti na wanadamu, Mungu hahisi amesongwa kufanya mambo kana kwamba anaishiwa na wakati. Akiwa “Mfalme wa umilele,” yeye anaona kila kitu vizuri sana na anaweza kuamua ni wakati gani, katika mkondo wa wakati, matendo yake yatawanufaisha zaidi wote wanaohusika.—1 Timotheo 1:17.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki