-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
‘MSUKUMO’ WAKATI WA MWISHO
15. Mfalme wa kusini ‘alimsukumaje’ mfalme wa kaskazini?
15 “Wakati wa mwisho mfalme wa kusini atashindana naye [“atamsukuma,” NW],” malaika akamwambia Danieli. (Danieli 11:40a) Je, mfalme wa kusini ‘amemsukuma’ mfalme wa kaskazini katika “wakati wa mwisho”? (Danieli 12:4, 9) Ndiyo, bila shaka. Baada ya vita ya ulimwengu ya kwanza, ule mkataba wa amani wa kumwadhibu mfalme wa kaskazini—Ujerumani—kwa kweli ‘ulimsukuma,’ ukimchochea alipize kisasi. Baada ya ushindi wake katika vita ya ulimwengu ya pili, mfalme wa kusini alimlenga mpinzani wake kwa makombora ya nyuklia yenye kuhofisha na kupanga muungano wa kijeshi wenye nguvu dhidi yake, Shirika la Kujihami la North Atlantic Treaty Organization (NATO). Kuhusu utendaji wa NATO, mwanahistoria mmoja Mwingereza asema hivi: “Ndicho kilichokuwa chombo kikuu cha ‘kuudhibiti’ [Muungano wa Sovieti], ambao sasa ulionwa kuwa tisho kuu la amani ya Ulaya. Lengo lake lilidumu kwa miaka 40, nalo lilitimizwa kwa mafanikio sana.” Miaka ya Vita Baridi ilipoendelea, kule ‘kusukumwa’ na mfalme wa kusini kulitia ndani upelelezi wa hali ya juu na vilevile mashambulio ya kidiplomasia na ya kijeshi.
-
-
Wafalme Washindani Wakaribia Mwisho WaoSikiliza Unabii wa Danieli!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 279]
‘Kusukuma’ kunakofanywa na mfalme wa kusini kumetia ndani upelelezi wa hali ya juu na utendaji wa kijeshi
-