-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuzimu na Jehanamu
Maana: Maneno “kuzimu” na “jehanamu” yanapatikana katika tafsiri nyingi za Biblia. Mahali ambapo neno “kuzimu” hutumiwa katika Biblia hizo, tafsiri nyingine hutumia neno “kaburi.” Biblia nyingine hutohoa tu maneno ya lugha za kwanza ambayo mara nyingine yanatafsiriwa “kuzimu”; yaani, zinatumia herufi za alfabeti zetu lakini zikiyaacha maneno hayo bila kutafsiriwa. Ni maneno gani hayo? Ni neno she’ohlʹ la Kiebrania, pamoja na haiʹdes, la Kigiriki, ambayo yanamaanisha, si kaburi la mtu mmoja, bali kaburi la ujumla la wafu;
-
-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Ayu. 14:13, UV: “[Ayubu alisali hivi:] Laiti ungenificha kuzimuni,* ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita, na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!” (Mungu mwenyewe alisema kwamba Ayubu alikuwa “mtu asiye na lawama na mnyoofu, mwenye kumwogopa Mungu na kujiepusha na ubaya.”—Ayu. 1:8.) (*“Hadeze,” ZSB; “Sheoli,” NW, kielezi-chini.)
-
-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
(1) Tafsiri ya Union Version ilitafsiri neno she’ohlʹ kuwa “kuzimu,” “kaburi,” na “shimo,”; haiʹdes limetafsiriwa humo kuwa “kuzimu”;
-
-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mhu. 9:5, 10: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe . . . Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi,* mahali unapokwenda.” (Ikiwa hawajui lolote, bila shaka hawahisi maumivu.) (*“Sheoli,” VB; “kaburi,” ZSB; “kuzimu,” UV.)
-