Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dumisheni Muungano Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
    • Utumie Ulimi Sawasawa!

      9. Ulimi unaweza kutumiwaje ili kuendeleza muungano?

      9 Kuutumia ulimi ili kuwatia wengine moyo ni njia ya maana ya kuendeleza muungano na roho ya udugu. Ile barua iliyosuluhisha swali juu ya tohara, kama ilivyotumwa na baraza linaloongoza la karne ya kwanza, ilikuwa chanzo cha kitia-moyo. Baada ya kuisoma, wanafunzi Wasio Wayahudi katika Antiokia ‘walitiwa moyo, wakafurahi.’ Yuda na Sila, waliokuwa wametumwa kutoka Yerusalemu wakiwa na barua hiyo, “walizungumza na hao ndugu kwa muda mrefu wakiwatia moyo na kuwaimarisha.” Pasipo shaka, kuwapo kwa Paulo na Barnaba pia kuliwatia moyo na kuwaimarisha ndugu wenzao katika Antiokia. (Matendo 15:1-3, 23-32, HNWW) Twaweza kufanya vivyo hivyo tunapokusanyika kwa ajili ya mikutano ya Kikristo na ‘kutiana moyo’ kupitia kuwapo kwetu na maelezo yetu yenye kujenga.—Waebrania 10:24, 25, NW.

  • Dumisheni Muungano Katika Siku Hizi za Mwisho
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
    • 11. Kwa nini unyenyekevu ni wa maana ikiwa tumesema jambo fulani ambalo limesababisha mkazo kati yetu na mwamini mwenzetu?

      11 Kuuzuia ulimi hutusaidia kudumisha muungano. (Yakobo 3:10-18) Lakini tuseme kwamba jambo fulani ambalo tumesema linasababisha mkazo kati yetu na Mkristo mwenzetu. Je, isingefaa kuchukua hatua ya kwanza katika kufanya amani na ndugu yetu, tukiomba msamaha ikiwa lazima? (Mathayo 5:23, 24) Ni kweli, jambo hilo lataka unyenyekevu, au hali ya akili ya kujishusha chini, lakini Petro aliandika hivi: “Jifungeni unyenyekevu [“hali ya akili ya kujishusha chini,” NW], mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.” (1 Petro 5:5) Unyenyekevu utatusukuma ‘tutafute amani’ pamoja na ndugu zetu, tukikiri makosa yetu na kuomba msamaha ifaavyo. Hilo husaidia kudumisha muungano wa familia ya Yehova.—1 Petro 3:10, 11.

      12. Twaweza kuutumiaje ulimi ili kuendeleza na kudumisha muungano wa watu wa Yehova?

      12 Twaweza kuendeleza roho ya familia miongoni mwa wale walio katika tengenezo la Yehova tukitumia ulimi wetu sawasawa. Kwa kuwa hivyo ndivyo Paulo alivyofanya, yeye aliweza kuwakumbusha Wathesalonike hivi: “Kama mjuavyo, jinsi tulivyomwonya kila mmoja wenu kama baba awaonyavyo watoto wake mwenyewe, tukiwatia moyo na kushuhudia; ili mwenende kama ilivyo wajibu wenu kwa Mungu.” (1 Wathesalonike 2:11, 12) Akiwa ameweka kielelezo chema kuhusu jambo hili, Paulo aliweza kuwahimiza Wakristo wenzake ‘waseme kwa kuliwaza nafsi zilizoshuka moyo.’ (1 Wathesalonike 5:14, NW) Ebu fikiria yale mema mengi tuwezayo kufanya kwa kuutumia ulimi ili kuwaliwaza, kuwatia moyo, na kuwajenga wengine. Ndiyo, “neno linenwalo wakati wa kufaa ni jema kama nini!” (Mithali 15:23) Zaidi ya hayo, usemi wa aina hiyo husaidia kuendeleza na kudumisha muungano wa watu wa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki