-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
‘Kuteswa milele’ kunakotajwa katika Ufunuo kunamaanisha nini?
Ufu. 14:9-11; 20:10, UV: “Mtu awaye yote akimsujudu huyo mnyama na sanamu yake, na kuipokea chapa katika kipaji cha uso wake, au katika mkono wake, yeye naye atakunywa katika mvinyo ya ghadhabu ya Mungu iliyotengenezwa, pasipo kuchanganywa na maji, katika kikombe cha hasira yake; naye atateswa kwa moto na kiberiti mbele ya malaika watakatifu, na mbele za Mwana-Kondoo. Na moshi wa maumivu [Kigiriki, basa·ni·smouʹ] yao hupanda juu hata milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake.”
-
-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Maandiko hayo yanazungumzia ‘kuteswa’ gani? Inafaa kutambua kwamba andiko la Ufunuo 11:10 (UV) linataja ‘manabii wanaotesa wao wakaao juu ya nchi.’ Mateso hayo yanatokana na ujumbe ambao manabii hao wanatangaza, unaofichua mambo kwa njia yenye kuaibisha. Andiko la Ufunuo 14:9-11 (UV) linasema kwamba wamsujudiao ‘mnyama huyo wa mfano na sanamu yake, wanateswa kwa moto na kiberiti.’ Hilo haliwezi kurejelea kuteswa kwa watu wenye fahamu baada ya kifo kwa sababu “wafu hawajui neno lo lote.” (Mhu. 9:5, UV) Basi, ni nini kinachowatesa wakiwa wangali hai? Ni lile tangazo linalotolewa na watumishi wa Mungu la kwamba wamsujudiao “mnyama na sanamu yake” watapatwa na kifo cha pili, kinachofananishwa na “ziwa la moto na kiberiti.” Moshi, unaohusianishwa na uharibifu wao unaofananishwa na moto, unaendelea kupanda milele kwa sababu uharibifu huo utakuwa wa milele na hautasahauliwa kamwe.
-