-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
‘Kuteswa milele’ kunakotajwa katika Ufunuo kunamaanisha nini?
Ufu. 14:9-11; 20:10, UV:
-
-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
“Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uwongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele.”
-
-
Kuzimu na JehanamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Andiko la Ufunuo 20:10 humaanisha nini linaposema kwamba Ibilisi ‘atateswa milele na milele’ katika “ziwa la moto na kiberiti”? Andiko la Ufunuo 21:8 (UV) husema waziwazi kwamba “lile ziwa la moto na kiberiti” humaanisha “kifo cha pili.” Kwa hiyo, ‘kuteswa’ kwa Ibilisi humo milele na milele kunamaanisha kwamba hatapata kitulizo kamwe; atazuiwa milele, katika kifo cha milele. Matumizi ya neno hilo ‘kuteswa’ (kutokana na neno la Kigiriki baʹsa·nos) humkumbusha mtu matumizi yake katika Mathayo 18:34, ambamo neno hilohilo la msingi la Kigiriki linatafsiriwa “watesaji” (UV, ZSB, VB), “walinzi wa jela” (NW), na “askari wa gereza” (NAJ).
-