Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waangalizi Wasafirio—Zawadi Zikiwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 15
    • 3. Kwa nini waangalizi wasafirio huhitaji kuwa na roho ya kujidhabihu?

      3 Waangalizi wasafirio husafiri sikuzote. Hilo lenyewe hutaka roho ya kujidhabihu. Mara nyingi kusafiri kutoka kutaniko moja hadi jingine kwaweza kuwa jambo gumu, lakini wanaume hao pamoja na wake zao hufanya hivyo wakiwa na mtazamo wenye shangwe. Mwangalizi wa mzunguko mmoja alisema hivi: “Mke wangu ni mwenye kuunga mkono kabisa na halalamiki . . . Anastahili kusifiwa sana kwa sababu ya roho yake ya kujidhabihu.” Waangalizi fulani wa mzunguko husafiri kilometa zaidi ya 1,000 kati ya makutaniko. Wengi huendesha magari, lakini wengine husafiri mahali-mahali kwa kutumia usafiri wa umma, baiskeli, farasi, au miguu. Mwangalizi wa mzunguko mmoja wa Afrika huhitaji hata kupitia mtoni akiwa amembeba mkewe mabegani pake ili kufikia kutaniko moja. Katika safari zake za umishonari, mtume Paulo alilazimika kukabiliana na joto na baridi, njaa na kiu, usiku kadhaa bila usingizi, hatari mbalimbali, na mnyanyaso wenye jeuri. Alikuwa pia na hali ya “kuhangaikia makutaniko yote”—jambo lililo la kawaida kwa waangalizi wasafirio leo.—2 Wakorintho 11:23-29.

      4. Matatizo ya afya yaweza kuwa na matokeo gani katika maisha za waangalizi wasafirio na wake zao?

      4 Sawa na Timotheo, mwandamani wa Paulo, nyakati nyingine waangalizi wasafirio na wake zao huwa na matatizo ya kiafya. (1 Timotheo 5:23) Hayo huwawekea mkazo wa ziada. Mke wa mwangalizi wa mzunguko mmoja aeleza hivi: “Kuwa pamoja na akina ndugu sikuzote ni mkazo ninapokuwa mgonjwa. Nikiwa nimefikia mwanzo wa komahedhi, nimeona hilo kuwa jambo gumu hasa. Kuhitaji kufunga tu vitu vyetu vyote kila juma na kuhamia kwingineko ni jambo gumu kwelikweli. Mara nyingi, inanibidi nitue na kusali kwa Yehova anipe nguvu za kuendelea.”

  • Waangalizi Wasafirio—Zawadi Zikiwa Wanadamu
    Mnara wa Mlinzi—1996 | Novemba 15
    • 11. Kwa nini tuwajulishe wake wa waangalizi wa mzunguko na wa wilaya kwamba wanapendwa na kuthaminiwa?

      11 Mke wa mwangalizi asafiriye kwa hakika hunufaika kutokana na maneno ya pongezi. Yeye ametoa dhabihu kubwa ili kumsaidia mumewe katika sehemu hii ya utumishi. Dada hawa waaminifu hujinyima tamaa ya asili ya kuwa na nyumba yao wenyewe, na pia katika visa vingi, ya kuwa na watoto. Binti Yeftha alikuwa mmoja wa watumishi wa Yehova aliyeacha kwa utayari fursa yake ya kuwa na mume na familia kwa sababu ya nadhiri aliyoweka babaye. (Waamuzi 11:30-39) Dhabihu yake ilionwaje? Waamuzi 11:40 lataarifu hivi: ‘Binti za Israeli walienda mwaka baada ya mwaka ili kumkumbuka huyo mwana wa Yeftha, Mgileadi, siku nne katika mwaka.’ Ni jambo zuri kama nini tujitahidipo kuwaambia wake wa waangalizi wa mzunguko na wa wilaya kwamba wanapendwa na kuthaminiwa!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki