-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Hivyo, Isaya anatimiza utume wake wa kiunabii, yaani, “kuwaagizia hao waliao katika Sayuni, wapewe taji ya maua badala ya majivu, mafuta ya furaha badala ya maombolezo, vazi la sifa badala ya roho nzito; wapate kuitwa miti [“mikubwa,” “NW”] ya haki [“uadilifu,” “NW”], iliyopandwa na BWANA, ili atukuzwe.”—Isaya 61:3.
-
-
Uadilifu Wachipuka Katika SayuniUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
12, 13. (a) Ni akina nani waliokuwa ‘miti mikubwa ya haki’ miongoni mwa Wayahudi wenye kurudi mwaka wa 537 K.W.K.? (b) Ni akina nani ambao wamekuwa ‘miti mikubwa ya haki’ tangu Pentekoste ya 33 W.K.?
12 Yehova anawabariki watu wake kwa kuwapa ‘miti mikubwa ya haki.’ Miti hiyo mikubwa ni akina nani? Katika miaka iliyofuata mwaka wa 537 K.W.K., miti hiyo ilikuwa watu mmoja-mmoja waliojifunza Neno la Mungu na kulitafakari, kisha wakasitawisha viwango vya Yehova vya uadilifu. (Zaburi 1:1-3; Isaya 44:2-4; Yeremia 17:7, 8) Wanaume kama vile Ezra, Hagai, Zekaria, na Kuhani Mkuu Yoshua walionekana hakika kwamba wao ni ‘miti mikubwa’ ya kutokeza—watu walio imara kuitetea kweli na kupinga uchafuzi wa kiroho katika taifa hilo.
13 Kuanzia Pentekoste ya 33 W.K. na kuendelea, Mungu alipanda ‘miti mikubwa ya haki’ kama hiyo, yaani Wakristo watiwa-mafuta walio na moyo mkuu. Aliwapanda katika makao ya kiroho ya taifa lake jipya, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Baada ya karne nyingi kupita, hatimaye idadi ya “miti” hiyo imekuwa 144,000, na inazaa matunda ya uadilifu ili kumrembesha, au kumtukuza, Yehova Mungu. (Ufunuo 14:3) Wale wa mwisho wa “miti” hiyo yenye fahari wamesitawi katika miaka ya tangu 1919, wakati Yehova alipowahuisha mabaki wa Israeli wa Mungu kutoka kwenye hali yao ya kutotenda kwa muda. Kwa kuwapa maji tele ya kiroho, inaweza kusemwa kwamba Yehova ametokeza msitu wa miti ya haki, yenye kuzaa matunda.—Isaya 27:6.
-