Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yajapokuwa Majaribu, Shikeni Imani Yenu!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 15
    • 12. Tunapopatwa na janga, kwa nini tusiseme: “Mimi ninajaribiwa na Mungu”?

      12 Je, yawezekana kwamba Yehova mwenyewe hutujaribu kwa janga? La, hatupaswi kusema: “Mimi ninajaribiwa na Mungu.” Yehova hajaribu kutufanya tutende dhambi lakini kwa hakika atatusaidia na kutupatia nguvu ihitajiwayo ili kuvumilia majaribu ikiwa tutaendelea kuwa imara katika imani. (Wafilipi 4:13) Mungu ni mtakatifu, kwa hiyo hatuweki katika hali ambazo zingedhoofisha kukinza kwetu utendaji-kosa. Tukijiingiza katika hali isiyo takatifu na kufanya dhambi fulani, tusimlaumu, “kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote.” Ingawa huenda Yehova akaruhusu jaribu litutie nidhamu kwa faida yetu, yeye hatujaribu akiwa na nia yenye uovu. (Waebrania 12:7-11) Huenda Shetani akatushawishi tufanye kosa, lakini Mungu aweza kutukomboa kutokana na mwovu huyo.—Mathayo 6:13.

  • Yajapokuwa Majaribu, Shikeni Imani Yenu!
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 15
    • 14. Zawadi za Mungu zaweza kusemwa kuwa ‘kamilifu’ katika maana gani?

      14 Twapaswa kukumbuka kwamba Yehova ndiye Chanzo cha vitu vyema, wala si cha majaribu. (Yakobo 1:16-18) Yakobo awaita waamini wenzake ‘ndugu wapendwa’ naye aonyesha kwamba Mungu ndiye Mpaji wa ‘kila zawadi njema na upaji mkamilifu.’ Zawadi za Yehova za kiroho na za kimwili ni ‘kamilifu,’ au kamili, zisizokosa chochote. ‘Zatoka juu,’ kutoka kwa makao ya Mungu mbinguni. (1 Wafalme 8:39) Yehova ndiye “Baba wa mianga ya kimbingu”—jua, mwezi, na nyota. Pia yeye hutupatia nuru na kweli ya kiroho. (Zaburi 43:3; Yeremia 31:35; 2 Wakorintho 4:6) Tofauti na jua ambalo hufanya vivuli vibadilike lizungukapo na liwapo kwenye upeo wake adhuhuri kamili tu, Mungu huwa katika kilele chake sikuzote akiandaa vitu vilivyo vyema. Kwa hakika atatuandalia vifaa vya kukabili majaribu tukitumia vizuri kabisa maandalizi yake ya kiroho yatolewayo kupitia Neno lake na “mtumwa [wake] mwaminifu na mwenye busara.”—Mathayo 24:45.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki