-
Tuyaoneje Majaribu?Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
-
-
Majaribu hutusaidia kusitawisha sifa nyingine pia—uvumilivu. Mwanafunzi Yakobo alisema; “Fikirieni yote kuwa shangwe, ndugu zangu, mkutanapo na majaribu ya namna mbalimbali, kama mjuavyo kwamba ubora huu uliojaribiwa wa imani yenu hutokeza uvumilivu.” (Yakobo 1:2, 3) Tukifanikiwa kuvumilia majaribu mbalimbali kwa kumtegemea Yehova kabisa, tutasitawisha sifa kama uimara, uthabiti, na uaminifu-maadili. Kufanya hivyo pia hutuimarisha kukinza mashambulio ya wakati ujao ya Shetani, mungu wa ulimwengu huu mwenye hasira.—1 Petro 5:8-10; 1 Yohana 5:19; Ufunuo 12:12.
-
-
Tuyaoneje Majaribu?Mnara wa Mlinzi—2002 | Septemba 1
-
-
Tunapata baraka nyingi pia tunapodumisha uaminifu-mshikamanifu wakati wa majaribu. Biblia inasema hivi kuhusu wale walio na tumaini la kwenda mbinguni: “Mwenye furaha ni mtu afulizaye kuvumilia jaribu, kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji la uhai, ambalo Yehova aliahidi wale waendeleao kumpenda.” (Yakobo 1:12)
-