Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mipango Yako Itafanywa Imara”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
    • ‘Mkabidhi Yehova Kazi Zako’

      Kufanya mipango kunahusisha kufikiri, jambo linalofanywa na moyo wetu. Kwa kawaida matendo yanafuata mipango. Je, mipango yetu itafaulu? Sulemani anasema: “Mkabidhi Yehova mwenyewe kazi zako nayo mipango yako itafanywa imara.” (Methali 16:3) Kumkabidhi Yehova kazi zetu kunamaanisha kumtumaini, kumtegemea yeye, kujitiisha kwake, kuacha kubeba mzigo wetu na badala yake kumkabidhi Yehova mzigo huo. Mtunga-zaburi aliimba hivi: “Mkabidhi Yehova njia yako, na kumtegemea, naye mwenyewe atatenda.”—Zaburi 37:5.

      Hata hivyo, ili mipango yetu ifanywe imara, ni lazima ipatane na Neno la Mungu na ichochewe na nia nzuri. Zaidi ya hilo, tunapaswa kumwomba Yehova atusaidie na kututegemeza kisha tujitahidi tuwezavyo kufuata mashauri ya Biblia. Ni muhimu hasa ‘tumtupie Yehova mzigo wetu’ tunapopatwa na majaribu na matatizo, kwa kuwa ‘atatutegemeza sisi.’ Bila shaka, Yehova “hatamwacha kamwe mwadilifu atikisike.”—Zaburi 55:22.

  • “Mipango Yako Itafanywa Imara”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Mei 15
    • “Huenda Moyo wa Mtu wa Udongo Ukaifikiria Njia Yake”

      Mwanadamu aliumbwa akiwa na uhuru wa kujiamulia, uwezo wa kuchagua mema au mabaya. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20) Moyo wetu wa mfano una uwezo wa kuchunguza mambo mbalimbali na kufuatia jambo moja au zaidi. Akionyesha kwamba daraka la kufanya uamuzi ni letu sisi, Sulemani anasema: “Huenda moyo wa mtu wa udongo ukaifikiria njia yake.” Baada ya hilo, “Yehova ndiye huzielekeza hatua zake.” (Methali 16:9) Kwa kuwa Yehova anaweza kuongoza hatua zetu, tunatenda kwa hekima tunapomwomba atusaidie ‘kufanya mipango yetu iwe imara.’

      Kama tulivyoona, moyo ni mdanganyifu na unaweza kuwa na mawazo yasiyo ya kweli. Kwa mfano, huenda mtu akafanya dhambi na moyo wake ukaanza kumtetea. Badala ya kuacha mwendo wake wenye dhambi, huenda akasema Mungu ni mwenye upendo, fadhili, rehema, na mwenye kusamehe. Mtu kama huyo amesema moyoni mwake: “Mungu amesahau. Ameuficha uso wake. Hakika hatauona kamwe.” (Zaburi 10:11) Hata hivyo, ni jambo lisilofaa na la hatari kuchezea rehema za Mungu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki