-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Hata hivyo, kwa sababu ya vita vilivyopiganwa kwa miaka kumi, kulikuwa na silaha nyingi mikononi mwa watu wafidhuli. Milio ya risasi na unyang’anyi yalikuwa mambo ya kawaida. Kwa tahadhari, wahubiri wa habari njema walijikakamua kueneza kotekote katika eneo magazeti na vitabu vyetu vya Biblia vyenye ujumbe wenye kufariji. Kwa wastani, kila mhubiri aligawa magazeti 12.5 mwezi wa Julai. Hata hivyo, kwa busara, utumishi wa shambani, sawa na shughuli nyingine, ulifanywa mchana kwa sababu usiku kulikuwa na hatari chungu nzima. Licha ya hatari zote hizo, ilionekana wazi kwamba kutakuwa na ongezeko.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
“Sikuzote tulifurahia kuwahubiria watu habari njema,” asema Marianne. “Walipenda mambo ya dini, walikuwa na Biblia, nao walikuwa tayari kusikiliza. Walikuwa wenye urafiki na adabu. Na licha ya hali ngumu za kiuchumi na nyinginezo, walikuwa na tabasamu sikuzote.”
-