-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Baadaye, Gilbert na Joan Walters walipewa mgawo wa kuhamia Jinja, ambako kazi ya kuhubiri haikuwa imefanywa vizuri.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Kwa mfano, huko Jinja, tayari ndugu wenyeji walikuwa wakihubiri pamoja na wamishonari. Jumapili walikuwa wakihubiri nyumba kwa nyumba kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa nne. Kisha, ziara za kurudia kwa saa moja na kuongoza funzo la Biblia mpaka saa sita. Kwa kufanya hivyo, wote kutanikoni walifaidika kutokana na uzoefu wa kila mmoja na kutiana moyo.
Kwa kuwa Jinja, mji wa pili kwa ukubwa nchini, una kituo cha kuzalishia umeme, ni eneo lenye viwanda vingi. Wamishonari walipata matokeo mazuri kwa kuhubiri katika vituo vya magari ya umma. Wasafiri kutoka mbali walikubali magazeti na vitabu vya Biblia ambavyo walivisoma wakiwa safarini. Hivyo, mbegu ya Ufalme ilienezwa hadi vijijini.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KUWASAIDIA WAHUBIRI WAPYA
Wakati huo kikundi cha Jinja kilikuwa kikifanyia mikutano yao katika jumba la umma katika mtaa wa Walukuba. “Ndugu wengi walikuwa wapya,” akumbuka Tom Cooke, “nao walikuwa na vichapo vichache ambavyo wangeweza kutumia kutayarishia migawo yao.” Msaada ungetoka wapi?
“Wamishonari waliweka maktaba katika nyumba ya ndugu mmoja aliyekuwa akiishi katikati ya mtaa huo,” asema Tom. “Kila Jumatatu (Siku ya 1) usiku, waliokuwa na migawo walienda kwa ndugu huyo kutumia maktaba ili kutayarisha hotuba zao.” Leo, kuna makutaniko mengi Jinja yanayoendelea na kazi ya uvuvi wa kiroho katika eneo hilo ambalo ni chanzo cha Mto Nile.
-