-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Makutaniko mengi nchini Uganda sasa hufanyia mikutano yao katika Jumba la Ufalme, nayo yameona faida ya kuwa na jumba lao wenyewe. Kwa kawaida ni rahisi zaidi kwa watu wanaopendezwa kuja mahali rasmi pa ibada badala ya kwenda katika darasa, na kwa sababu hiyo hudhurio limeongezeka nayo makutaniko yamekua sana.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
SEHEMU ZAIDI ZA IBADA ZAHITAJIWA
Zamani, mikutano ilikuwa ikifanyiwa katika nyumba za watu, vituo vya umma, na madarasa. Majengo ya kwanza kutumiwa kwa kusudi pekee la mikutano ya Kikristo yalikuwa majengo ya matofali yaliyoezekwa kwa nyasi sehemu za vijijini huko Namaingo na Rusese. Bila shaka jitihada za ndugu hao zilibarikiwa katika maeneo hayo mawili, na makutaniko yakasitawi huko.
-