-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ndiyo sababu, kufikia mwaka wa 2003, kulikuwa na wahubiri wa Ufalme zaidi ya 3,000 nchini Uganda, na miaka mitatu tu baadaye, mwaka wa 2006, idadi hiyo ilifikia 4,005.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Makutaniko mengi nchini Uganda sasa hufanyia mikutano yao katika Jumba la Ufalme, nayo yameona faida ya kuwa na jumba lao wenyewe. Kwa kawaida ni rahisi zaidi kwa watu wanaopendezwa kuja mahali rasmi pa ibada badala ya kwenda katika darasa, na kwa sababu hiyo hudhurio limeongezeka nayo makutaniko yamekua sana.
KUSHUGHULIKIA ONGEZEKO LA HARAKA
Ongezeko la haraka la makutaniko lilifanya iwe vigumu kupata mahali panapofaa kwa ajili ya makusanyiko. Ni nini kingeweza kufanywa ili kupata mahali panapofaa ambapo pangepunguza uhitaji wa kusafiri mbali, hasa kwa akina ndugu wa vijijini? Utatuzi ulipatikana wakati kibali kilipotolewa cha kujenga Majumba ya Ufalme yanayoweza kupanuliwa. Hayo ni majumba ya kawaida lakini yenye eneo la nje lenye paa na sakafu tu bila kuta za kando. Sehemu ya nyuma ya Jumba la Ufalme inapofunguliwa, eneo hilo lenye paa linaweza kutoshea watu wengi zaidi wakati wa kusanyiko. Majumba kama hayo yamejengwa Kajansi, Rusese, na Lira, na la nne linaendelea kujengwa Seta.
Yehova amebariki ukuzi wa kiroho nchini Uganda na kwa sababu hiyo mabadiliko ya kitengenezo yamehitajika. Kabla ya mwaka wa 1994, kulikuwa na mzunguko mmoja tu nchi nzima. Baadaye, mizunguko zaidi ilianzishwa ili kushughulikia idadi yenye kuongezeka ya makutaniko na vikundi na lugha mbalimbali zinazotumika. Leo, kukiwa na makutaniko 111 na vikundi 50, Uganda ina mizunguko nane, mitatu ikiwa ya Kiganda.
-