-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Mwaka wa 1958 wahubiri wakaanza kutumia kijitabu “Habari Njema Hizi za Ufalme” kilichokuwa kimetafsiriwa karibuni. Hilo lilikuwa jambo lenye kutia moyo kama nini! Kazi ilisonga mbele na katika mwaka wa 1961, kulikuwa na kilele kipya cha wahubiri 19.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Hata hivyo, muda usio mrefu baadaye, kazi ya Ufalme ikapata pigo. Baadhi ya ndugu kutoka nchi za kigeni walirudi makwao baada ya kandarasi zao kwisha. Ndugu kadhaa walitengwa na ushirika, na wengine wakakwazwa na mienendo isiyopatana na Maandiko ya watu fulani kutanikoni.
-