-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
KUSHINDA VIPINGAMIZI
Hata hivyo, pamoja na maendeleo ya miaka ya mwisho-mwisho ya 1980 kulikuwa na magumu pia. Mnamo Julai 1985, kulikuwa na mapinduzi mengine ya kijeshi. Kama awali, hali ya usalama ikazorota, vita vya wanamgambo vikapamba moto. Majeshi yaliyotimuliwa yakaanza kupora mali na kuwapiga watu risasi ovyoovyo. Kwa muda, kulikuwa na mapambano makali karibu na makao ya wamishonari mjini Jinja. Siku moja makao yao yalivamiwa na wanajeshi, hata hivyo wavamizi hao walipopata kuwatambua wamishonari, hawakuharibu chochote badala yake walichukua vitu vichache sana. Kisha, Januari 1986, serikali nyingine tena ikashika hatamu na kujaribu kurejesha utulivu nchini.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Miaka ya 1980 ilipokuwa ikikaribia mwisho, watu walikuwa na matumaini makubwa nchini Uganda. Hali ya usalama ilikuwa ikirejea, nao uchumi wa nchi ulikuwa ukifufuka. Miundo-msingi iliboreshwa, na miradi mbalimbali ya kijamii ikaanzishwa upya au kutekelezwa.
-