Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uganda
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • FURSA NA MATATIZO MAPYA

      Mwaka wa 1980, Ndugu Reschke alizuru makao makuu huko Brooklyn, New York. Akiwa huko aliombwa atoe ripoti kuhusu Uganda. Baadaye, washiriki wa Baraza Linaloongoza walitaja kwamba kuna uwezekano wa kutuma tena wamishonari Uganda. Ulikuwa wakati barabara wa kufanya hivyo, kwa kuwa kwa mara nyingine tena ingewezekana kukusanyika pamoja nchini Uganda. Isitoshe, kufikia mwaka wa 1981 kulikuwa na wahubiri 175, na mwezi wa Julai mwaka huohuo, Uganda ilifurahi kuwa na kilele kipya cha wahubiri 206.

  • Uganda
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • WAMISHONARI WAKARIBISHWA TENA

      Wahitimu wa Shule ya Gileadi, Jeffrey Welch na Ari Palviainen waliwasili Kampala kutoka Kenya mnamo Septemba 1982. Tangu mwanzo, Jeff na Ari walipata matokeo mazuri. “Watu walikuwa na njaa ya mambo ya kiroho,” akumbuka Jeff, “kwa hiyo magazeti yakiwa na habari zenye kuvutia, ‘yalijiangusha.’”

      Mwezi wa Desemba, Heinz na Marianne Wertholz, kutoka katika Tanzu la Shule ya Gileadi huko Wiesbaden, Ujerumani, walijiunga na Jeff na Ari. Tangu mwanzo, akina Wertholz walichochewa sana na bidii ya ndugu zao wa Uganda licha ya kwamba walikuwa wakiishi katika hali mbovu na hatari.

      “Huduma nyingi,” akumbuka Heinz, “kama vile maji na mawasiliano zilikuwa zimezorota. Kulikuwa na migogoro ya kisiasa. Mara kadhaa kulikuwa na uvumi wa kwamba serikali itapinduliwa, na wanajeshi waliweka vizuizi vingi barabarani. Milio ya risasi na unyang’anyi yalikuwa mambo ya kawaida hasa wakati wa usiku. Giza lilipoingia, barabara zilikuwa tupu. Kila mtu alikaa nyumbani akitumaini—na mara nyingi kusali—kwamba usiku utapita salama.”

      Heinz na Marianne walikaa na familia ya Sam Waiswa huku wakiendelea kutafuta nyumba ambayo ingekuwa makao ya wamishonari. Ijapokuwa Sam alikuwa na taaluma ya kufundisha, hali za kiuchumi nchini humo zilikuwa zimewalemea sana hivi kwamba ukarimu wa familia yake kwa kweli haukuwa na kifani.

      “Haikuwa rahisi kupata nyumba mahali salama,” asema Heinz, “kwa hiyo tulikaa kwa Sam kwa miezi mitano. Katika kipindi hicho tulipata kufahamiana vizuri. Nyakati nyingine walikuwa wakila mlo mmoja tu kwa siku, hata hivyo, walikuwa na furaha sikuzote; nao watoto walikuwa watiifu na wenye heshima. Kwa kuwa maji ya jiji hayakutegemeka, watoto hao walikuwa wakienda kuteka maji kwa mitungi ya lita 20 na kuyabeba kichwani. Tuliporudi nyumbani kutoka shambani, sikuzote kulikuwa na maji ya kutumia. Bila shaka, tulijifunza kuhifadhi maji. Kwa mfano, tulitumia kiasi kidogo cha maji tulipooga, na kuyahifadhi ili yatumike vyooni.”

      Mwezi wa Aprili 1983, miaka kumi baada ya wamishonari wa mwisho kuondoka nchini Uganda, wamishonari hao wanne wapya walipata makao mapya mahali palipokuwa salama kiasi. Ukosefu wa usalama na upungufu wa vitu ulifanya hali iwe ngumu, hata hivyo, upendo wa ndugu wenyeji ulifanya wasahau yote hayo.

      “Sikuzote tulifurahia kuwahubiria watu habari njema,” asema Marianne. “Walipenda mambo ya dini, walikuwa na Biblia, nao walikuwa tayari kusikiliza. Walikuwa wenye urafiki na adabu. Na licha ya hali ngumu za kiuchumi na nyinginezo, walikuwa na tabasamu sikuzote.”

  • Uganda
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • “MTU HUSEMAJE . . . ?”

      Miaka ya 1980, wahubiri wenye bidii nchini Uganda waliwakaribisha wamishonari wenye hamu waliozidi kumiminika nchini. Baadhi yao walikuwa wamishonari wapya waliohitimu kutoka Shule ya Gileadi, na wengine walilazimika kutoka katika migawo yao ya umishonari nchini Zaire (ambako leo ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo). Kwa kuwa sasa kulikuwa na idadi kubwa ya wamishonari mjini Kampala na Jinja, maeneo yenye watu wengi yangeweza kuhubiriwa kikamili zaidi, nao wamishonari walifurahi kuona kwamba eneo la Uganda lilikuwa tayari kuvunwa. Shida haikuwa kuwapata watu wanaopendezwa na ujumbe wetu, bali kuwasaidia kufanya maendeleo.

      Akiwa ametoka tu katika Shule ya Gileadi, Mats Holmkvist alikuwa na bidii sana, naye alikuwa na hamu ya kujifunza lugha ya wenyeji ili kuwasaidia watu wapendezwe na kweli. Wakati huo, Fred Nyende alikuwa painia wa pekee mjini Entebbe, naye aliutumia ujuzi wake wa kutafsiri na ukalimani kuwafundisha wamishonari kuzungumza kwa ufasaha Kiganda, lugha ambayo nyakati nyingine maneno yake huwa magumu kutamka. Mats alitoa jasho.

      “Mtu husemaje, ‘Ufalme wa Mungu’ katika Kiganda?” akauliza Mats mwanzoni-mwanzoni mwa masomo yake.

      “Obwakabaka bwa Katonda,” akamjibu Fred, kana kwamba yuaimba.

      ‘Jamani,’ akawaza Mats huku akighairi kwamba laiti hangeuliza. Hata hivyo, Mats alipiga hatua kubwa na hatimaye aliweza kukizungumza Kiganda vizuri.

  • Uganda
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • 1963 Wamishonari wawasili.

  • Uganda
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • 1973 Mashahidi wa Yehova wapigwa marufuku na wamishonari wafukuzwa.

  • Uganda
    2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • 1982 Wamishonari waruhusiwa tena kuingia nchini.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki