-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Muda mfupi baadaye, akina Smith walimhubiria Peter Gyabi, aliyekuwa na cheo katika serikali ya Uganda, pamoja na mke wake, Esther. Awali, Peter alikuwa amepata kitabu What Has Religion Done for Mankind?b lakini hakukisoma kwa makini kwa sababu ya shughuli zake nyingi kazini na kuhamishwa-hamishwa kikazi. Kisha, siku moja Peter alitumwa kutatua mzozo wa shamba kati ya makabila mawili. Alisali, “Mungu, iwapo utanisaidia, nitakutafuta.” Utatuzi ulipopatikana kwa amani, alikumbuka sala yake, naye akaanza kukisoma kile kitabu. Alitambua mambo aliyokuwa akijifunza ni kweli naye akaanza kuwatafuta Mashahidi. Alifurahi sana alipokutana na Frank Smith, aliyekubali kumfundisha yeye na mke wake Biblia kwa ukawaida! Wenzi hao wa ndoa wenye furaha walibatizwa, nao bado ni wahubiri wenye bidii wa Ufalme, zaidi ya miaka 40 baadaye.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 77]
Upendo wa Kweli wa Kikristo Wagusa Mioyo
PETER GYABI
ALIZALIWA 1932
ALIBATIZWA 1965
MAELEZO MAFUPI KUMHUSU Mzee wa kutaniko aliyesaidia katika kazi ya kutafsiri wakati wa marufuku. Yeye na mke wake Esta, wana watoto wanne ambao ni watu wazima sasa.
◼ WAMISHONARI wa kwanza Mashahidi wa Yehova walipofika Uganda, kulikuwa na ubaguzi wa rangi nchini, nao wazungu wengi hawakuchangamana na watu weusi. Upendo wa kweli wa wamishonari uligusa mioyo yetu, nasi tukawapenda sana.
Katika miaka ya 1970, tulifurahia kuhubiri na kushirikiana na wamishonari waliokuwa wakiishi Mbarara, kilomita 65 hivi kutoka kwetu. Siku moja, tulipokuwa tukienda kuwatembelea, wanajeshi walitusimamisha. Mmoja wao akatuambia: “Ikiwa mnataka kufa, endeleeni na safari yenu.” Tukaamua kurudi. Baada ya siku kadhaa, tukaanza kuwa na wasiwasi kuhusu wamishonari hao. Tulitaka sana kufika wanakoishi ili kuwajulia hali. Kulikuwa na ulinzi mkali sana. Nililazimika kutumia cheo changu katika hospitali na kibandiko cha hospitali kwenye gari kupita vizuizi vya barabarani. Tulifurahi sana kuwapata wamishonari hao wakiwa salama. Tuliwanunulia vyakula na kukaa nao siku kadhaa. Kisha tukawa tukiwatembelea kila juma mpaka kulipokuwa na usalama wa kutosha kuhamia Kampala. Kadiri hali zilivyozidi kuwa ngumu, ndivyo tulivyozidi kujionea upendo wa kindugu.
-