-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Makabiliano mengine na polisi hayakuwa yenye kuogopesha sana. Kwa mfano, familia ya Emmanuel Kyamiza na mke wake, pamoja na kikundi kidogo cha watu wenye kupendezwa, walikuwa wakifanya mikutano kisiri nyumbani kwao mjini Entebbe. Ili kuepuka kugunduliwa, Emmanuel alikuwa akibadili mahali pa kuongozea mafunzo ya Biblia. Baada ya muda, Emmanuel akadhani kwamba mbinu zake za kuwakwepa polisi zinafaulu. Siku moja, baada ya Emmanuel kumaliza kuongoza funzo la Biblia katika bustani inayoitwa Entebbe Botanical Gardens, polisi mmoja alianza kutembea kuelekea mahali alipokuwa huku naye akijaribu kuficha vitabu vyake visionekane. “Mbona unaficha vitabu vyako?” akauliza polisi huyo. “Tunajua mnalofanya. Tunajua ninyi ni Mashahidi wa Yehova. Hata tunajua mahali mnapokutanikia. Ikiwa tungetaka, tungekuwa tumewakamata kitambo sana. Lakini mnaweza kuendelea na mambo yenu.” Naye Emmanuel akaendelea—kwa uaminifu!
Baadaye, Emmanuel alipostaafu na kurudi kijijini kwao, aliendelea kuvumilia upinzani na dhihaka. Kama Yesu, ‘hakuheshimiwa katika eneo la nyumbani.’ (Marko 6:4) Hata hivyo, hata kufikia alipokuwa na umri wa miaka 70 na kitu, Emmanuel aliendelea “kusitawi wakati wa kuwa na kichwa chenye mvi,” naye alikuwa akiendesha baiskeli yake na kusafiri umbali wa kilomita 30 ili kuhudhuria mikutano. (Zab. 92:14) Leo, akiwa na umri wa miaka 80 na kitu, angali anatumikia kwa uaminifu akiwa mtumishi wa huduma, ijapokuwa haendeshi sana baiskeli yake kama zamani.
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 96]
Emmanuel Kyamiza
-