-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
George na Gertrude Ochola walikuwa miongoni mwa wenyeji waliohudhuria. Gertrude anasema: “Hilo lilikuwa kusanyiko langu la kwanza, ambapo nilibatizwa!” Lakini George hakuwa Shahidi wakati huo. Alikuwa shabiki wa soka naye alipendezwa zaidi na uwanja wenyewe. Hata hivyo, mwishowe alijiweka wakfu na kubatizwa mwaka wa 1975 nchini Kenya, baada ya kujifunza Biblia na pia kuchochewa na mwenendo mzuri wa mke wake.
Gertrude anakumbuka kwamba alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kujifunza kweli kutoka sehemu za kaskazini za Uganda. “Mwaka wa 1972, nilipobatizwa,” asema, “nilidhani kwamba kwetu ni mbali sana. Lakini leo, kuna Jumba la Ufalme, makao ya wamishonari, na hata ofisi ya kutafsiri. Hilo hunisisimua sana kuliko nilipobatizwa!”
-
-
Uganda2010 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 90]
George na Gertrude Ochola
-