Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuwaelimisha Wasikilizaji
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Ni vizuri kufafanua mambo kwa njia rahisi. Watu wengine hushangaa kujifunza maana ya “ufalme” unaotajwa katika Mathayo 6:10. Ufafanuzi wa jambo hata unaweza kumsaidia Mkristo wa zamani kufahamu vizuri maana ya andiko fulani. Jambo hili ni wazi unaposoma 2 Petro 1:5-8 na kufafanua sifa zinazotajwa katika mistari hiyo: imani, wema wa adili, ujuzi, kujidhibiti, uvumilivu, ujitoaji-kimungu, shauku ya kidugu, na upendo. Ikiwa maneno yanayofanana yanatumiwa katika muktadha uleule, unaweza kuyafafanua ili kutofautisha maana ya neno moja na jingine. Ndivyo ilivyo kuhusu maneno kama hekima, maarifa, ufahamu, na busara ambayo yametumiwa katika Mithali 2:1-6.

  • Kuwaelimisha Wasikilizaji
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Msemaji akitaja wakati kitabu fulani cha Biblia kilipoandikwa au wakati tukio fulani lilipotokea, anapaswa pia kufafanua hali zilizokuwako wakati huo. Kwa njia hiyo, wasikilizaji wataelewa kwa urahisi zaidi umuhimu wa kitabu hicho au tukio hilo.

  • Kuwaelimisha Wasikilizaji
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    • Namna gani kama hotuba yako inazungumzia baadhi ya “mambo yenye kina kirefu ya Mungu”? (1 Kor. 2:10) Ukianza kwa kutenganisha na kufafanua mambo makuu, wasikilizaji wataelewa kwa urahisi mambo madogo-madogo. Na ukimalizia kwa muhtasari mfupi, wasikilizaji wanaweza kuridhika kwamba kweli wamejifunza kitu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki