-
“Bwana Huwapa Watu Hekima”Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
-
-
Tunawezaje ‘kuita uelewevu’—uwezo wa kutambua jinsi sehemu mbalimbali za habari fulani zinavyohusiana kwa jumla? Bila shaka, umri na uzoefu ni mambo yawezayo kutusaidia tusitawishe uelewevu zaidi—lakini nyakati nyingi haiwi hivyo. (Ayubu 12:12; 32:6-12) “Ninao ufahamu kuliko wazee,” akasema mtunga-zaburi, “kwa kuwa nimeyashika mausia yako [Yehova].” Pia aliimba hivi: “Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga [“asiye na uzoefu,” NW].” (Zaburi 119:100, 130) Yehova ndiye “mzee wa siku,” naye ana uelewevu mkubwa zaidi kushinda binadamu yeyote. (Danieli 7:13) Mungu anaweza kumpa uelewevu mtu asiye na uzoefu, akimwezesha kuwa na uelewevu mwingi zaidi kushinda wazee. Hivyo, yatupasa kujitahidi kujifunza na kutumia Neno la Mungu, Biblia.
-
-
“Bwana Huwapa Watu Hekima”Mnara wa Mlinzi—1999 | Novemba 15
-
-
Kujipatia uelewevu kwahitaji kutafakari jinsi habari mpya inavyopatana na yale ambayo tayari tunajua.
-