-
Hii Ndiyo Siku ya Wokovu!Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 15
-
-
12. Ni huduma gani muhimu ambayo inatekelezwa na mabalozi na wajumbe wa Yehova?
12 Ili kupata wokovu, ni lazima tutende kupatana na maneno ya Paulo: “Tukiwa tunafanya kazi pamoja naye [Yehova], twawasihi sana nyinyi pia msiipokee fadhili isiyostahiliwa ya Mungu na kukosa kusudi layo. Kwa maana yeye asema: ‘Wakati wenye kukubalika nilikusikia, na siku ya wokovu nilikusaidia.’ Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:1, 2) Mabalozi wa Yehova watiwa-mafuta na wajumbe wake, “kondoo wengine,” hawakubali fadhili isiyostahiliwa ya Baba yao wa kimbingu na kukosa kusudi lake. (Yohana 10:16) Kwa mwenendo wao mwadilifu na huduma yao yenye bidii katika “wakati [huu] wenye kukubalika,” wao wanatafuta upendeleo wa Mungu na wanawaarifu wakazi wa dunia kwamba hii ndiyo “siku ya wokovu.”
-
-
Hii Ndiyo Siku ya Wokovu!Mnara wa Mlinzi—1998 | Desemba 15
-
-
15. Tangu lini Waisraeli wa kiroho wamejitahidi kuthibitika kuwa wastahili fadhili ya Mungu isiyostahiliwa, na kwa lengo gani?
15 Paulo atumia andiko la Isaya 49:8 kuwarejezea Wakristo watiwa-mafuta, akiwasihi ‘wasikose kusudi la fadhili isiyostahiliwa ya Mungu’ kwa kushindwa kutafuta nia njema yake katika “wakati wenye kukubalika” na “siku ya wokovu” aandaayo. Paulo aongeza kusema: “Tazameni! Sasa ndio wakati wenye kukubalika hasa. Tazameni! Sasa ndiyo siku ya wokovu.” (2 Wakorintho 6:2) Tangu Pentekoste mwaka wa 33 W.K., Waisraeli wa kiroho wamejitahidi kuthibitika kuwa wastahili fadhili ya Mungu isiyostahiliwa ili “wakati wenye kukubalika” uwe “siku ya wokovu” kwao.
-