-
Yehova Hatakuacha Hata KidogoMnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
-
-
Adam, baba Mkristo mwenye watoto wawili, anaeleza jinsi alivyohisi alipofutwa kazi: “Nilikasirika haraka; na kila kitu kiliniudhi. Hata usiku niliota kuhusu kazi na jinsi ya kutosheleza mahitaji ya watoto wangu na mke wangu ambaye pia alikuwa amesimamishwa kazi ghafula.” Ryszard na Mariola, wenzi wa ndoa walio na mtoto mmoja, walipopoteza njia yao ya kupata riziki, walikuwa na deni kubwa la benki. Mariola anasema: “Kila wakati nilisumbuka kihisia, dhamiri yangu ilinifanya nihisi kwamba nilikosea kuchukua mkopo huo. Nilikuwa nikijilaumu.”
-
-
Yehova Hatakuacha Hata KidogoMnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
-
-
Hivyo ndivyo Adam aliyetangulia kutajwa alivyohisi. Anasema: “Mimi na mke wangu tulipofutwa kazi, hatukuwahi kufikiria kuacha kuhudhuria mikutano ya Kikristo au kupunguza bidii yetu ya kuhubiri. Mtazamo huo ulitusaidia kutohangaika sana kuhusu kesho.” Ryszard ana maoni kama hayo, anasema: “Kama si mikutano na huduma, hatungeweza kuvumilia; bila shaka tungemezwa na mahangaiko. Kuzungumzia mambo ya kiroho pamoja na wengine hututia moyo, kwa sababu hutufanya tuwahangaikie badala ya kujihangaikia.”—Wafilipi 2:4.
-
-
Yehova Hatakuacha Hata KidogoMnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
-
-
Utafanyaje hivyo? Adam anaeleza: “Usikae kitako ukingojea Mungu akusaidie au afanye muujiza. Unapotafuta kazi, usisite kujitambulisha kuwa Shahidi wa Yehova. Waajiri huthamini hilo.” Ryszard anatoa shauri hili: “Muulize yeyote unayemjua kuhusu nafasi za kazi, endelea kuulizia kazi kwenye mashirika ya kuwatafutia watu kazi, soma matangazo ya kazi, kama yale yanayosema: ‘Tunatafuta mwanamke wa kumtunza mlemavu’; au ‘Kazi ya muda: Kuchuna kahawa.’ Usichoke kutafuta kazi! Usichague-chague kazi, hata ikiwa utalazimika kufanya kazi ya hali ya chini au isiyopatana na miradi yako.”
-
-
Yehova Hatakuacha Hata KidogoMnara wa Mlinzi—2005 | Oktoba 15
-
-
Adam na Irena walipata riziki kwa kuosha madirisha na ngazi, na hawakutumia pesa ovyoovyo. Pia, walitembelea kwa ukawaida vituo vya kuwatafutia watu kazi. Irena anasema: “Sikuzote tulipata msaada tulipouhitaji.” Mume wake anaongeza: “Tumekuja kugundua kwamba mambo fulani tuliyotaja katika sala zetu hayakupatana na mapenzi ya Mungu. Hilo limetufunza kutegemea hekima ya Mungu na kutotenda kulingana na uelewaji wetu. Ni afadhali kutulia na kungoja suluhisho kutoka kwa Mungu.”—Yakobo 1:4.
Ryszard na Mariola walifanya kazi mbalimbali za hali ya chini na wakati huohuo wakahubiri katika maeneo yenye uhitaji mkubwa. Ryszard anasema: “Tulipata kazi tulizohitaji wakati ambapo hatukuwa na chakula chochote. Tulikataa kazi zenye mshahara mnono ambazo zingehitilafiana na utendaji wetu wa kitheokrasi. Tuliona ni afadhali kumngojea Yehova.” Wanaamini kwamba Yehova aliongoza mambo na kuwawezesha kukodi nyumba kwa bei nafuu na hatimaye Ryszard akapata kazi.
-