-
Fumbo Lenye Kutia Hofu LafumbuliwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Amani na Usalama —Tumaini la Bure
10, 11. (a) UM ulipiga mbiu ya nini katika 1986, na itikio lilikuwa nini? (b) Ni “jamaa za kidini” ngapi zilizokusanyika katika Assisi, Italia, kusali kwa ajili ya amani, na je! Mungu anajibu sala kama hizo? Fafanua.
10 Katika jitihada za kutegemeza matumaini ya aina ya binadamu, Umoja wa Mataifa ulipiga mbiu ya 1986 kuwa “Mwaka wa Amani ya Kimataifa,” ukiwa na kichwa “Kulinda Salama Amani na Wakati Ujao wa Binadamu.” Mataifa yenye kupiga vita yaliombwa yalaze silaha zayo, angalau kwa mwaka mmoja. Itikio layo lilikuwa nini? Kulingana na ripoti iliyotolewa na Taasisi ya Utafiti wa Amani ya Kimataifa, watu wapatao milioni tano walikufa kwa sababu ya vita wakati wa 1986 pekee! Ingawa sarafu kadhaa za pekee na stampu za mwadhimisho zilitolewa, mataifa yaliyo mengi yalifanya kidogo sana kwa habari ya kufuatia wazo bora la amani katika mwaka huo. Hata hivyo, dini za ulimwengu—zikitamani sikuzote kuafikiana na UM—zilianza kutangaza mwaka huo kwa njia mbalimbali. Katika Januari 1, 1986, Papa John Paul 2 alisifu kazi ya UM na akaweka wakfu mwaka mpya kwa ajili ya amani. Na katika Oktoba 27, akakusanya viongozi wa nyingi za dini za ulimwengu katika Assisi, Italia, ili kusali kwa ajili ya amani.
11 Je! Mungu anajibu sala kama hizo kwa ajili ya amani? Basi, viongozi wa kidini hao walikuwa wakisali kwa Mungu yupi? Kama ungewauliza, kila kikundi kingekupa jibu tofauti. Je! kuna jamii ya mamilioni ya miungu inayoweza kusikia na kujibu maombi rasmi yaliyotolewa kwa njia nyingi mbalimbali? Wengi wa washiriki waliabudu Utatu wa Jumuiya ya Wakristo.c Wabuddha, Wahindu, na wengine walitoa sala zao kwa miungu isiyo na hesabu. Kwa ujumla, “jamaa za kidini” 12 zilikusanyika, zikiwa zinawakilishwa na watu mashuhuri kama Askofu Mkuu wa Kianglikana wa Kantabari, Dalai Lama wa Buddha, kasisi wa Orthodoksi la Urusi, Msimamizi wa Ushirika wa Patakatifu pa Shinto wa Tokyo, waabudu-mizimu wa Kiafrika, na Wahindi Waamerika wawili waliovalia vazi la kichwani la manyoya-manyoya. Kilikuwa kikundi chenye rangi za namna namna, bila kusema zaidi, kikifanyiza kipindi cha TV chenye kutazamisha. Kikundi kimoja kilisali bila kukoma kwa saa 12 katika wakati mmoja. (Linga Luka 20:45-47.) Lakini je! yoyote ya sala hizo ilipenya mawingu ya mvua yaliyoning’inia juu ya mkusanyiko huo? Kwa sababu zinazofuata, la:
12. Ni kwa sababu zipi Mungu hakujibu sala za viongozi wa kidini wa ulimwengu kwa ajili ya amani?
12 Tofauti na wale ambao “hutembea katika jina la Yehova,” hakuna mwanadini hata mmoja wa hao aliyekuwa akisali kwa Yehova, Mungu aliye hai, ambaye jina lake huonekana mara zapata 7,000 katika maandishi asilia ya Biblia. (Mika 4:5; Isaya 42:8, 12, NW)d Wakiwa kikundi wao hawakumwendea Mungu kwa jina la Yesu, walio wengi wao wakiwa hata hawaitikadi katika Yesu Kristo. (Yohana 14:13; 15:16) Hakuna baadhi yao wanaofanya mapenzi ya Mungu kwa ajili ya siku yetu, ambayo ni kupiga mbiu ulimwenguni pote ya Ufalme unaokuja wa Mungu—si UM—kuwa ndilo tumaini halisi kwa aina ya binadamu. (Mathayo 7:21-23; 24:14; Marko 13:10) Kwa sehemu iliyo kubwa zaidi matengenezo ya kidini yao yamejihusisha katika vita vyenye umwagaji-damu vya historia, kutia na vita viwili vya ulimwengu vya karne ya 20. Kwa hao, Mungu husema: “Hata ingawa nyinyi mnafanya sala nyingi, mimi sisikilizi; mikono yenu imejawa na umwagaji-damu.”—Isaya 1:15, NW; 59:1-3.
13. (a) Ni kwa nini ni jambo la maana kwamba viongozi wa kidini wa ulimwengu wamepaswa kuungana mikono na UM katika kutoa mwito kwa ajili ya amani? (b) Vilio kwa ajili ya amani vitafikia upeo gani uliotabiriwa kimungu?
13 Na zaidi, ni jambo la maana yenye kina kwamba viongozi wa kidini wamepaswa kuungana mikono na Umoja wa Mataifa katika kutoa mwito kwa ajili ya amani wakati huu. Wao wangependa kutumia uvutano juu ya UM kwa faida yao wenyewe, hasa katika enzi hii ya ki-siku-hizi wakati watu wao wanaacha dini. Kama viongozi wasio waaminifu katika Israeli wa kale, wao wanalia, “‘Kuna amani! Kuna amani!’ wakati hakuna amani.” (Yeremia 6:14, NW) Pasipo shaka vilio vyao kwa ajili ya amani vitaendelea, vikiwa vinainuka katika kuunga mkono upeo ambao kuhusu huo mtume Paulo alitolea unabii: “Siku ya Yehova inakuja sawasawa kama mwivi katika usiku. Wakati wowote wanaposema: ‘Amani na usalama!’ ndipo uharibifu wa ghafula utakuwa juu yao papo hapo kama maumivu makali ya ghafula ya taabu juu ya mwanamke mwenye mimba; na wao hawataponyoka kwa vyovyote.”—1 Wathesalonike 5:2, 3, NW.
14. Huenda kilio cha “Amani na usalama!” kitakuwa cha namna gani, na mmoja anaweza kuepukaje kuongozwa vibaya?
14 Katika miaka ya hivi karibuni, wanasiasa wametumia maneno “amani na usalama” kuelezea mipango mbalimbali ya wanadamu. Je! jitihada hizo za viongozi wa ulimwengu zinaonyesha mwanzo wa utimizo wa andiko la 1 Wathesalonike 5:3? Au je, Paulo alikuwa akizungumzia tukio hususa na lenye kutokeza sana hivi kwamba lingetambuliwa ulimwenguni? Kwa kuwa mara nyingi unabii wa Biblia hueleweka kikamili tu baada ya kutimia au wakati unapoendelea kutimia, itatubidi tungoje tuone itakuwaje. Kwa sasa, Wakristo wanajua kwamba hata ingawa huenda ikaonekana kana kwamba mataifa yamepata amani na usalama, hakuna kitu ambacho kwa kweli kitakuwa kimebadilika. Ubinafsi, chuki, uhalifu, mvunjiko wa jamaa, ukosefu wa adili, magonjwa, huzuni, na kifo bado vitakuwapo. Ndiyo sababu si lazima wewe uongozwe vibaya na kilio chochote cha “amani na usalama,” ikiwa umeamka kuona maana ya matukio ya ulimwengu na unatii maonyo ya kiunabii katika Neno la Mungu.—Marko 13:32-37; Luka 21:34-36.
-
-
Fumbo Lenye Kutia Hofu LafumbuliwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 250]
Kinyume cha “Amani”
Ingawa 1986 ulipigiwa mbiu na UM kuwa Mwaka wa Amani ya Kimataifa, shindano la ujiuaji la kuunda silaha liliongezeka. World Military and Social Expenditures 1986 hutoa fasili hizi zenye kumakinisha:
Katika 1986 matumizi ya kijeshi ya tufe lote yalifikia dola milioni elfu 900.
Matumizi ya kijeshi ya tufe lote ya saa moja yangetosha kuchanja watu milioni 3.5 ambao walikufa kila mwaka kutokana na magonjwa ya kuambukiza yenye kuzuilika.
Ulimwenguni pote, mtu mmoja kati ya watano aliishi katika umaskini wenye kuumiza. Watu hao wote wenye kufa-njaa wangeweza kulishwa kwa mwaka mmoja kwa gharama ya kile kiasi ambacho ulimwengu ulitumia kwa ajili ya silaha katika siku mbili.
Nishati ya baruti iliyo katika rundo la silaha za nyukilia za ulimwengu ilikuwa kubwa zaidi ya ule mlipuko wa Chernobyl kwa mara 160,000,000.
Bomu moja la nyukilia lingeweza kupelekwa likiwa na nguvu za mlipuko mara zaidi ya 500 ya bomu lililoangushwa juu ya Hiroshima katika 1945.
Maghala ya zana za nyukilia yalikuwa na nguvu za baruti zinazolingana na Hiroshima zaidi ya milioni moja. Yaliwakilisha mara 2,700 za nguvu za baruti zilizoachiliwa katika Vita ya Ulimwengu 2, wakati watu milioni 38 walikufa.
Vita vilikuwa vikitokea mara nyingi zaidi na ni vyenye kufisha zaidi. Vifo kutokana na vita vilikuwa jumla ya milioni 4.4 katika karne ya 18, milioni 8.3 katika karne ya 19, milioni 98.8 katika miaka 86 ya kwanza ya karne ya 20. Tangu karne ya 18, vifo kutokana na vita vimeongezeka zaidi ya mara sita kuliko idadi ya watu ya ulimwengu. Kulikuwako vifo mara kumi kwa kila vita katika karne ya 20 kuliko ilivyokuwa katika karne ya 19.
-