-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
20. (a) Yohana anaonyeshaje kwamba kwa mara nyingine tena Yehova atatumia watawala wa kibinadamu kutekeleza hukumu? (b) “Fikira” ya Mungu ni nini? (c) Ni katika njia gani mataifa yatafikiliza “fikira moja,” yayo lakini kwa kweli ni fikira ya nani itatimizwa?
20 Kwa mara nyingine tena Yehova anatumia watawala wa kibinadamu kutekeleza hukumu. “Kwa maana Mungu alitia hilo ndani ya mioyo yao kufikiliza fikira yake, hata kufikiliza fikira yao moja kwa kumpa ufalme wao hayawani-mwitu, mpaka hapo maneno ya Mungu yatakuwa yametimilizwa.” (Ufunuo 17:17, NW) “Fikira” ya Mungu ni nini? Kupangia wafishaji wa Babuloni Mkubwa waungane pamoja, ili kumharibu kabisa. Bila shaka, matilaba ya watawala katika kumshambulia yatakuwa kufikiliza “fikira moja” yao wenyewe. Wao watahisi kwamba ni kwa masilahi yao ya utukuzaji wa taifa kumgeukia huyo kahaba mkubwa. Huenda wakaja kuona kule kuendelea kwa dini iliyopangwa kitengenezo ndani ya mipaka yao kuwa tisho kwa enzi zao. Lakini Yehova atakuwa kwa kweli akiongoza mambo kwa werevu; wao watafikiliza fikira yake kwa kuharibu kwa dharuba moja adui yake mzinzi wa muda mrefu!—Linga Yeremia 7:8-11, 34.
21. Kwa kuwa hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu atatumiwa katika kuharibu Babuloni Mkubwa, kwa wazi mataifa yatafanya nini kwa habari ya Umoja wa Mataifa?
21 Ndiyo, mataifa yatatumia hayawani-mwitu rangi-nyekundu-nyangavu, Umoja wa Mataifa, katika kuharibu Babuloni Mkubwa. Wao hawatendi kwa utangulizi wao wenyewe, kwa maana Yehova hutia ndani ya mioyo yao “hata kufikiliza fikira moja yao kwa kumpa ufalme wao hayawani-mwitu.” Wakati ujapo, kwa wazi mataifa yataona uhitaji wa kuimarisha Umoja wa Mataifa. Itakuwa kana kwamba, wanaupa meno, wakiupa mamlaka yoyote na nguvu waliyo nayo ili kwamba uweze kugeukia dini bandia na kupiga vita kwa kufaulu dhidi yayo “mpaka hapo maneno ya Mungu yatakuwa yametimilizwa.” Hivyo, kahaba wa kale atakuja kwenye mwisho wake kabisa. Na apotelee mbali!
-
-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Si mataifa yale tu, kama yanavyowakilishwa na pembe kumi, yanayomharibu kahaba mkubwa, bali pia “hayawani-mwitu,” kumaanisha UM wenyewe, hujiunga nayo katika kuonyesha jeuri hii. Utatoa idhini yao ili dini bandia iharibiwe. Yaliyo mengi ya yale mataifa 190 na zaidi yaliyo ndani ya UM yameonyesha tayari, kwa kiolezo chayo cha kupiga kura, uhasama wayo kuelekea dini, hasa ile ya Jumuiya ya Wakristo.
-
-
Kufisha Babuloni MkubwaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Na pembe kumi ambazo wewe uliona, na hayawani-mwitu, hizi zitachukia kahaba na zitafanya yeye kuwa mwenye kuteketezwa na mwenye uchi, na zitakula kabisa sehemu zake zenye mnofu na zitachoma yeye kabisa kabisa kwa moto.’”—Ufunuo 17:15, 16, NW.
-