-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kurekebisha Sheria ya Kikatiba
Katika nchi nyingine, utendaji wa Mashahidi wa Yehova umekuwa jambo kuu katika kurekebisha sheria. Kila mwanafunzi wa sheria wa Amerika ajua vema sehemu waliyoshiriki Mashahidi wa Yehova katika kutetea haki za raia katika Marekani. Makala zilizoonyesha kadiri ya ushiriki huo ni kama zifuatazo: “Deni la Sheria ya Kikatiba kwa Mashahidi wa Yehova,” iliyotokea katika Minnesota Law Review, la Machi 1944, na, “Kisababishi cha Marekebisho ya Sheria ya Kikatiba: Mashahidi wa Yehova Katika Mahakama Kuu Zaidi,” iliyochapwa katika University of Cincinnati Law Review, katika 1987.
Kesi zao za mahakamani hufanyiza sehemu kubwa ya sheria za Marekani zinazohusu uhuru wa dini, uhuru wa usemi, na uhuru wa uandishi. Kesi hizo zimeshiriki sehemu kubwa katika kudumisha uhuru si wa Mashahidi wa Yehova tu bali pia wa watu wote. Katika hotuba kwenye Chuo Kikuu cha Drake, mwandishi na mhariri mashuhuri, Irving Dilliard, alisema: “Upende usipende, Mashahidi wa Yehova wamefanya mengi katika kusaidia kudumisha uhuru wetu kuliko kikundi kingine chochote cha kidini.”
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 699]
“Utumishi kwa Lengo la Kupata Uhuru wa Kidini”
“Isingekuwa haki kupuuza pitio hili fupi la matatizo ya Mashahidi wa Yehova na Serikali bila kurejezea utumishi kwa lengo la kupata uhuru wa kidini chini ya Katiba yetu ambao umetolewa kwa sababu ya kusisitiza kwao. Katika miaka ya karibuni wamechukua wakati mwingi wa mahakama kuliko kikundi kinginecho cha kidini, na kwa umma wameonekana kuwa wasio na akili, lakini wameshikamana na masadikisho yao ya kudhamiria, na kama tokeo mahakama za Taifa zimetoa mfululizo wa maamuzi ambayo yameleta na yakapanua uhakikisho wa uhuru wa kidini kwa raia wa Amerika, na yamelinda na kuongeza uhuru wao wa kiraia. Kesi zipatazo thelathini na moja ambazo walihusika zililetwa mbele ya Mahakama Kuu Zaidi katika miaka mitano kuanzia 1938 hadi 1943, na maamuzi ya kesi hizo na nyinginezo za baadaye yamesitawisha sana lengo la uhuru wa Haki za Msingi za Kibinadamu kwa ujumla, na kulindwa kwa uhuru wa kidini hasa.”—“Church and State in the United States,” cha Anson Phelps Stokes, Buku 3, 1950, ukurasa 546.
-