-
Kukabiliana na Magumu ya Eneo la PekeeAmkeni!—2004 | Januari 8
-
-
Jumba la Ufalme Katika Eneo la Pekee
Mnamo Jumamosi, Juni 7, 2003, Jumba la Ufalme la Chinle liliwekwa wakfu. Hotuba ya wakfu ilitolewa na Gerrit Lösch, mshiriki wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Alizungumza juu ya ongezeko kubwa la Majumba ya Ufalme ulimwenguni pote na kusema kwamba bado maelfu ya majumba mengine yanahitajiwa kwa ajili ya yale makutaniko zaidi ya 94,600. Pia aliwaeleza wahudhuriaji 165 waliokuwapo sababu 15 za kuthamini jumba lao jipya na faida za kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida. Alimalizia kwa sala ya wakfu, akimwomba Yehova abariki matumizi ya jumba hilo maridadi.
Zamani, kabla kutaniko hilo halijaanzishwa, lilikuwa kikundi cha Kutaniko la Keams Canyon, lililo umbali wa kilometa 100 hivi kusini-magharibi. Sasa Kutaniko la Chinle lina jukumu la kuhubiri habari njema za Ufalme wa Mungu katika eneo lenye ukubwa wa zaidi ya kilometa 11,000 za mraba! Wanavajo wengi huishi katika nyumba zinazoweza kuhamishwa zenye umbo la pembe sita au pembe nane. Gari linalokwenda kwa magurudumu yote manne linahitajiwa ili kuyafikia maeneo ya mbali, kama korongo la kupendeza la Canyon de Chelly (linatamkwa d’Shay).
-
-
Kukabiliana na Magumu ya Eneo la PekeeAmkeni!—2004 | Januari 8
-
-
Ukitembelea eneo la Canyon de Chelly, utapitia barabara ya Navajo Route 7. Kwenye kona iliyo karibu na Ishara ya Kitaifa, tafuta ishara inayosema “Jiihōvah Yádahalne’í bi Kingdom Hall” na “Kingdom Hall of Jehovah’s Witnesses.” Unakaribishwa kwenye jumba hilo.
-