-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Sasa, je, wanapaswa wafanye uchapaji wao wenyewe? Walijitahidi kununua matbaa-mabamba-mviringo ya kuchapa magazeti lakini waliambiwa kwamba kulikuwa na chache tu katika Marekani na kwamba kulikuwa hakuna uwezekano wa kupata moja kwa miezi mingi. Hata hivyo, walikuwa na uhakika kwamba ikiwa yalikuwa mapenzi ya Bwana, angeweza kufungua njia. Na alifanya hivyo!
Miezi michache tu baada ya wao kurudi Brooklyn, waliweza kununua matbaa-mabamba-mviringo. Walikodisha orofa tatu katika jengo moja lililokuwa umbali wa majengo manane kutoka Kao la Betheli, kwenye 35 Myrtle Avenue. Kufikia mapema 1920 Sosaiti ilikuwa na kiwanda chayo cha kuchapisha—kidogo, lakini chenye vifaa vingi. Ndugu waliokuwa na ujuzi wa kutosha kuendesha vifaa hivyo walijitoa wenyewe ili kusaidia katika kazi hiyo.
Toleo la Februari 1 la The Watch Tower mwaka huo lilichapwa kwa matbaa ya Sosaiti. Kufikia Aprili, The Golden Age pia lilikuwa likitolewa kwa matbaa yao wenyewe. Kufikia mwisho wa mwaka huo, ilikuwa furaha kwa The Watch Tower kuripoti: “Wakati wa sehemu kubwa ya mwaka kazi yote ya THE WATCH TOWER, THE GOLDEN AGE, na vijitabu vingi, ilikuwa imefanywa na mikono iliyojitakasa, lakini kusudi moja ndilo lililoelekeza vitendo vyao, na kusudi hilo ni kumpenda Bwana na kusudi lake la uadilifu. . . . Majarida mengine na vichapo yalipotakiwa kukoma kwa sababu ya upungufu wa karatasi au matatizo ya wafanyakazi, vichapo vyetu viliendelea kutokezwa bila tatizo.”
Nafasi kwenye kiwanda ilikuwa ndogo sana, lakini kiasi cha kazi kilichofanywa kilistaajabisha. Kiasi cha The Watch Tower kilichochapwa kilikuwa nakala 60,000 kwa kila toleo. Lakini The Golden Age lilichapwa huko pia, na katika mwaka wa kwanza, toleo la Septemba 29 lilikuwa la pekee. Lilikuwa na habari nyingi juu ya kufunuliwa kwa wachochezi wa mnyanyaso dhidi ya Wanafunzi wa Biblia kuanzia 1917 hadi 1920. Nakala milioni nne zilichapwa! Mmojawapo wafanyakazi wa matbaa ya kiwanda alisema hivi baadaye: ‘Kila mtu isipokuwa mpishi alitumikia ili kutokeza toleo hilo.’
Katika mwaka wao wa kwanza wa kutumia matbaa-mabamba-mviringo ya kuchapa magazeti, Ndugu Rutherford aliomba akina ndugu ikiwa wangeweza pia kuchapa vijitabu kwa matbaa hiyo. Mwanzoni, haikuonekana kuwa yawezekana. Wafanyakazi wa matbaa hiyo walisema kwamba haingewezekana. Lakini akina ndugu walijaribu na wakapata matokeo mazuri. Pia walifanyiza mashine yao wenyewe ya kukunja na hivyo wakapunguza uhitaji wa wafanyakazi katika sehemu hiyo ya kazi kutoka 12 hadi 2. Ni nini kilichowafanikisha? “Ujuzi na baraka ya Bwana” ndivyo msimamizi wa kiwanda alivyokata kauli.
Hata hivyo, haikuwa katika Brooklyn pekee kwamba Sosaiti ilikuwa ikianzisha shughuli za uchapaji. Baadhi za shughuli za uchapaji katika lugha za kigeni zilisimamiwa na ofisi katika Michigan. Ili kushughulikia mahitaji yaliyohusiana na kazi hiyo, Sosaiti ilipeleka mashine ya Linotaipu, matbaa za kuchapa, na vifaa vingine vilivyohitajika katika Detroit, Michigan katika 1921. Huko fasihi zilichapwa katika Kipoland, Kirusi, Kiukrainia, na lugha nyinginezo.
Katika mwaka uo huo, Sosaiti ilitoa kitabu The Harp of God, kilichoandikwa kwa njia inayofaa wale wanaoanza kujifunza Biblia. Kufikia 1921 Sosaiti haikuwa imejaribu kuchapa na kujalidi vitabu vyayo yenyewe. Je, wangepaswa kujitahidi kuanza kazi hiyo pia? Kwa mara nyingine, walitafuta mwelekezo wa Bwana.
Ndugu Waliojitoa Wachapa na Kujalidi Vitabu
Katika 1920, The Watch Tower lilikuwa limeripoti kwamba makolpota wengi walikuwa wamelazimika kuacha utumishi huo kwa sababu wachapaji na wajalidi wa vitabu walishindwa kufanyiza vitabu vilivyoagizwa na Sosaiti. Akina ndugu kwenye makao makuu walitoa sababu kwamba ikiwa hawangewategemea watengenezaji wa kibiashara wenye matatizo mengi ya kazi, wangetimiza ushahidi mwingi zaidi kuhusu makusudi ya Mungu kwa wanadamu. Ikiwa wangechapa na kujalidi vitabu vyao wenyewe, ingekuwa pia vigumu zaidi kwa wapinzani kuingilia kazi hiyo. Na baadaye walitumaini wangeweza kupunguza gharama ya kuchapa mabuku na hivyo waweze kuyafanya yapatikane kwa urahisi zaidi kwa umma.
Lakini hilo lingetaka nafasi na vifaa vingi zaidi, na wangelazimika kujifunza stadi mpya. Je, wangeweza kufanya hivyo? Robert J. Martin, mwangalizi wa kiwanda, alikumbuka kwamba katika siku za Musa, Yehova alikuwa ‘amewajaza Bezaleli na Oholiabu hekima ya moyoni ili waifanye kazi yote’ iliyohitajiwa katika kujenga tabenakulo takatifu. (Kut. 35:30-35) Akiwa na simulizi hilo la Biblia akilini, Ndugu Martin alikuwa na uhakika kwamba Yehova angeweza pia kufanya chochote kilichohitajiwa ili kwamba watumishi wake waweze kuchapa fasihi ili wautangaze Ufalme.
Baada ya kutafakari kwingi na sala nyingi, mipango hususa ilianza kutokea. Akitazama nyuma kwa yale yaliyotokea, Ndugu Martin alimwandikia Ndugu Rutherford baadaye hivi: “Siku iliyo kuu kupita zote ilikuwa ile siku ulipotaka kujua ikiwa kulikuwa na sababu yoyote nzuri kwa nini sisi hatupaswi kuchapa na kujalidi vitabu vyetu vyote. Lilikuwa wazo la kusisimua, kwa sababu lilimaanisha kufunguliwa kwa kiwanda kamili cha kupanga chapa, kupakaza kwa umeme, kuchapa na kujalidi, ikihitaji kuendesha mashine nyingi tusizofahamu, sanasana mashine ambazo hatukujua zilikuwako, na uhitaji wa kujifunza stadi nyingi. Lakini hiyo ilionekana kuwa ndiyo njia bora zaidi ya kupunguza gharama ya vitabu baada ya ile vita.
“Ulikodisha jengo la orofa sita kwenye barabara ya 18 Concord Street (kukiwa na wakazi katika orofa mbili); na mnamo Machi 1, 1922, tukahamia humo. Ulitununulia mashine kamili za kupanga chapa, kupakaza kwa umeme, kuchapa na kujalidi, nyingi zazo zikiwa mpya, baadhi yazo zikiwa zimetumiwa; na tukaanza kazi.
“Mojawapo kiwanda kikubwa cha uchapaji kilichokuwa kimekuwa kikifanya sehemu kubwa ya kazi yetu kilisikia yale tuliyokuwa tukifanya na msimamizi wa kiwanda hicho akaja, ili kutuzuru. Aliona vifaa vipya na akasema hivi kwa uzito, ‘Hapa mna kiwanda cha uchapaji kilicho bora zaidi, na hakuna yeyote katika kiwanda anayejua jinsi ya kukiendesha. Katika miezi sita kiwanda chote cha uchapaji kitakuwa takataka; na mtagundua kwamba watu wanaostahili kuwachapia ni wale ambao sikuzote wamekuwa wakiwachapia, wakiifanya iwe shughuli yao.’
“Hilo lilisikika kuwa jambo la akili vya kutosha, lakini lilisahau Bwana; na sikuzote amekuwa pamoja nasi. Ujalidi ulipoanza alimtuma ndugu ambaye ametumia maisha yake yote katika shughuli ya ujalidi. Alikuwa msaada mkubwa wakati alipohitajiwa zaidi. Kwa msaada wake, na roho ya Bwana ikitenda kazi miongoni mwa ndugu waliokuwa wakijaribu kujifunza, upesi tulianza kufanyiza vitabu.”
Kwa kuwa kiwanda kwenye barabara ya Concord Street kilikuwa na nafasi kubwa, shughuli za uchapaji kutoka Detroit ziliunganishwa na zile za Brooklyn. Kufikia mwaka wa pili katika sehemu hiyo, ndugu walikuwa wakifanyiza asilimia 70 ya vitabu na vijitabu vilivyohitajiwa, kutia na magazeti, trakti, na vikaratasi vya ukaribishaji. Mwaka uliofuata, walilazimika kutumia orofa mbili zilizobaki za kiwanda kwa sababu ya ukuzi wa kazi.
Je, wangeweza kuongeza mwendo wa kutokeza vitabu? Matbaa ya kuchapia ilitengenezwa katika Ujerumani, ikasafirishwa kwa meli hadi Amerika, na kuanza kufanya kazi katika 1926 hasa kwa kusudi hilo. Kwa kadiri walivyojua, matbaa hiyo ya kuchapa ndiyo iliyokuwa ya aina yake ya kwanza kutumiwa katika Amerika ili kuchapa vitabu.
-
-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Lakini, wakati wa kipindi cha mnyanyaso mwingi katika 1918, huku maofisa wa Sosaiti wakiwa wamefungwa isivyo haki, makao yao makuu (yaliyoko Brooklyn, New York) yalibomolewa. Mabamba ya kuchapia yaliharibiwa. Wafanyakazi waliopungua sana walihamisha ofisi kurudi Pittsburgh kwenye orofa ya tatu ya jengo moja katika 119 Federal Street. Je, hilo lingewazuia kutokeza fasihi za Biblia?
Je, Wapaswa Wafanye Uchapaji Wao Wenyewe?
Baada ya kuachiliwa kwa msimamizi wa Sosaiti, J. F. Rutherford, na washiriki wake kutoka gerezani, Wanafunzi wa Biblia walikusanyika katika Cedar Point, Ohio, katika 1919. Walifikiria yale ambayo Mungu alikuwa ameruhusu yatukie wakati wa mwaka uliotangulia na yale ambayo Neno lake lilionyesha kwamba wanapaswa kuwa wakifanya wakati wa siku zilizokuwa mbele. Tangazo lilitolewa kwamba gazeti jipya, The Golden Age, lingechapwa likiwa chombo cha kutumia katika kuelekeza watu kwa Ufalme wa Mungu ukiwa tumaini pekee la wanadamu.
Kama ilivyokuwa imefanya zamani, Sosaiti ilipanga ili mashirika ya kibiashara yachape. Lakini nyakati zilikuwa zimebadilika. Kulikuwa na matatizo ya wafanyakazi katika shughuli ya uchapaji na matatizo katika soko la karatasi. Mpango wenye kutegemeka zaidi ulihitajiwa. Ndugu walisali juu ya jambo hilo na wakawa macho kuona maelekezo ya Bwana.
-