-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Hatimaye, katika 1940, Mahakama ilisikiliza kikamili kesi iliyoitwa Minersville School District v. Gobitis.k Kundi kubwa la mawakili mashuhuri walitoa hoja katika kesi hiyo kwa pande zote. J. F. Rutherford alitoa hoja ya maneno kwa niaba ya Walter Gobitas na watoto wake. Mshiriki wa idara ya sheria ya Chuo Kikuu cha Harvard aliwakilisha Shirika la Mawakili wa Marekani na Chama cha Kutetea Uhuru wa Raia katika kutoa hoja dhidi ya kusalimu bendera kwa lazima. Hata hivyo, hoja zao zilikataliwa, na kukiwa na mmoja tu aliyekuwa na maoni tofauti, Mahakama Kuu Zaidi iliamua mnamo Juni 3, kwamba watoto ambao hawangesalimu bendera wangefukuzwa kutoka shule za umma.
-
-
“Kutetea na Kuthibitisha Kisheria Habari Njema”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Lillian na William Gobitas
-