-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Malinda Keefer alipozungumza na Ndugu Russell katika 1907 kuhusu tamaa yake ya kuanza utumishi wa wakati wote, alisema kwamba alihisi uhitaji wa kupata ujuzi zaidi kwanza. Kwa kweli, ni mwaka mmoja tu uliokuwa umepita alipoona fasihi za Wanafunzi wa Biblia kwa mara ya kwanza. Jibu la Ndugu Russell lilikuwa: “Ikiwa unataka ungoje hadi utakapoyajua yote hutaanza kamwe, bali utajifunza unapoendelea kuifanya.” Bila kusita, yeye alianza upesi katika Ohio, Marekani. Mara nyingi alikumbuka Zaburi 110:3, inayosema: “Watu wako wanajitoa kwa hiari.” Kwa miaka 76 iliyofuata, aliendelea kufanya ivyo hivyo.b Alianza utumishi huo akiwa mseja. Kwa miaka 15 alifurahia kutumikia akiwa ameolewa. Lakini baada ya mume wake kufa, aliendelea tu, kwa msaada wa Yehova. Akikumbuka muda wa miaka iliyopita, yeye alisema: “Nina shukrani kama nini kwamba nilijitoa kwa hiari kuwa painia nilipokuwa mwanamke mchanga na nikatanguliza masilahi ya Ufalme nyakati zote!”
-
-
“Kutafuta Kwanza Ufalme”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 285]
Kwa miaka 76—akiwa mseja, akiwa ameolewa, na kisha akiwa mjane—Malinda Keefer alijitoa mwenyewe kwenye huduma ya wakati wote
-