-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Robert J. Martin, mwangalizi wa kiwanda, alikumbuka kwamba katika siku za Musa, Yehova alikuwa ‘amewajaza Bezaleli na Oholiabu hekima ya moyoni ili waifanye kazi yote’ iliyohitajiwa katika kujenga tabenakulo takatifu. (Kut. 35:30-35) Akiwa na simulizi hilo la Biblia akilini, Ndugu Martin alikuwa na uhakika kwamba Yehova angeweza pia kufanya chochote kilichohitajiwa ili kwamba watumishi wake waweze kuchapa fasihi ili wautangaze Ufalme.
Baada ya kutafakari kwingi na sala nyingi, mipango hususa ilianza kutokea. Akitazama nyuma kwa yale yaliyotokea, Ndugu Martin alimwandikia Ndugu Rutherford baadaye hivi: “Siku iliyo kuu kupita zote ilikuwa ile siku ulipotaka kujua ikiwa kulikuwa na sababu yoyote nzuri kwa nini sisi hatupaswi kuchapa na kujalidi vitabu vyetu vyote. Lilikuwa wazo la kusisimua, kwa sababu lilimaanisha kufunguliwa kwa kiwanda kamili cha kupanga chapa, kupakaza kwa umeme, kuchapa na kujalidi, ikihitaji kuendesha mashine nyingi tusizofahamu, sanasana mashine ambazo hatukujua zilikuwako, na uhitaji wa kujifunza stadi nyingi. Lakini hiyo ilionekana kuwa ndiyo njia bora zaidi ya kupunguza gharama ya vitabu baada ya ile vita.
“Ulikodisha jengo la orofa sita kwenye barabara ya 18 Concord Street (kukiwa na wakazi katika orofa mbili); na mnamo Machi 1, 1922, tukahamia humo. Ulitununulia mashine kamili za kupanga chapa, kupakaza kwa umeme, kuchapa na kujalidi, nyingi zazo zikiwa mpya, baadhi yazo zikiwa zimetumiwa; na tukaanza kazi.
“Mojawapo kiwanda kikubwa cha uchapaji kilichokuwa kimekuwa kikifanya sehemu kubwa ya kazi yetu kilisikia yale tuliyokuwa tukifanya na msimamizi wa kiwanda hicho akaja, ili kutuzuru. Aliona vifaa vipya na akasema hivi kwa uzito, ‘Hapa mna kiwanda cha uchapaji kilicho bora zaidi, na hakuna yeyote katika kiwanda anayejua jinsi ya kukiendesha. Katika miezi sita kiwanda chote cha uchapaji kitakuwa takataka; na mtagundua kwamba watu wanaostahili kuwachapia ni wale ambao sikuzote wamekuwa wakiwachapia, wakiifanya iwe shughuli yao.’
“Hilo lilisikika kuwa jambo la akili vya kutosha, lakini lilisahau Bwana; na sikuzote amekuwa pamoja nasi. Ujalidi ulipoanza alimtuma ndugu ambaye ametumia maisha yake yote katika shughuli ya ujalidi. Alikuwa msaada mkubwa wakati alipohitajiwa zaidi. Kwa msaada wake, na roho ya Bwana ikitenda kazi miongoni mwa ndugu waliokuwa wakijaribu kujifunza, upesi tulianza kufanyiza vitabu.”
-
-
Kutokeza Fasihi za Biblia Ili Zitumiwe Katika HudumaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 580]
R. J. Martin, (kulia), mwangalizi wa kwanza wa kiwanda cha Sosaiti cha Brooklyn, akizungumza na Ndugu Rutherford
-